Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

UM yatoa mwito kwa pande zote Sierra Leone kuepusha ghasia kabla uchaguzi.

UM umetoa mwito kwa vyama vyote vya kisiasa huko Sierra Leone kujiepusha kutumia matusi na maneno ya uchochezi yanayoweza kusababisha ghasia kabla ya uchaguzi wa rais na wa bunge wa mwezi ujao. Mwakilishi maalum wa katibu mkuu Victor Angelo akizungumza katika kikao cha ufunguzi wa mkutano wa kitaifa juu ya majadiliano na vijana alisema, inabidi tufahamu matukiyo ya hivi karibuni ya ghasia za kisiaasa.

Mkutano juu ya mzozo wa Darfur unmepangwa kufanyika mapema Augusti.

Wajumbe maalum wa UM na AU wakiendelea na juhudi za kutafuta suluhisho la kisiasa kwa ajili ya ugomvi wa jimbo la Darfur huko Sudan, wamewaalika viongozi wa makundi ambayo hayakutia sahihi makubaliano ya amani kwa mazungumzo ya ‘majadiliano ya awali’ yaliyopangwa kuanza mapema mwezi ujao huko Arusha Tanzania.

Kwa habari za hapa na pale

Mashirika ya huduma za dharura ya UM yanapeleka kwa haraka misaada ya chakula na afya kusini mwa Sudan ambako mvua kali mnamo siku za hivi karibuni zimesababisha mafuriko yaliyowathiri karibu watu elfu 10. Shirika la watoto la UM, UNICEF limeshapeleka mikoba midogo 1 500 madawa na vitu vya dharura, pamoja na chakula cha siku 15.