Siku ya Kufyeka Malaria Afrika
Wiki hii, Jumuiya ya Ushirikiano wa Kurudisha Nyuma Malaria imewasilisha mradi mpya wa kufadhilia huduma za kupiga vita maradhi ya malaria Afrika. Jumuiya hiyo inatumai kwamba nusu ya maombi yote ya yale mataifa yanayohitajia msaada huo yatatekelezewa mataifa husika, hususan katika bara la Afrika, eneo ambalo, kila mwaka, asilimia 90 ya vifo milioni 1 vya malaria hutukia.