Mataifa ya KiAfrika na FAO yaahidi kuimarisha elimu vijijini
Mataifa 11 ya KiAfrika, yalikutana karibuni mjini Rome, Utaliana kwenye Makao Makuu ya Shirika la UM la Chakula na Kilimo (FAO) na yaliafikiana kushiriki kwenye ule mradi wa kuimarisha elimu ya msingi vijijini, kwa dhamira ya kusaidia wakazi wa maeneo hayo kujipatia ujuzi wa kupiga vita, kwa mafanikio, ufukara, matatizo ya njaa, utapia mlo na kutojua kusoma na kuandika. Maafa haya ya kijamii huathiri zaidi mataifa ya Afrika yaliopo kusini ya Sahara.