Yanayojadiliwa mkutanoni hayana tija yasipotekelezwa kwa vitendo mashinani: Madina Kimaro
Mkutano wa Umoja wa Mataifa wa mabadiliko ya tabianchi COP28 unakunja jamvi mjini Dubai Falme za nchi za Kiarabu. Wakuu wa nchi na serikali, wadau wa mazingira wanazuoni, asasi za kiraia na vijana kutoka mataifa 199 wamejadili mengi ikiwemo hatma ya kuhakikisha joto halizidi juzijoto 1.5 na mustakbali wa matumizi ya mafuta kisukuku.