Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Makala Maalum

Kundi la watu wenye ulemavu ambao wanashiriki Jukwaa la WEIF 2024
UN News/Abdelmonem Makki

Azimio la 5 la Manama lapitishwa, watu wenye ulemavu waonesha ubingwa wao kwenye ugunduzi

Azimio la 5 la Manama limepitishwa hii leo huko Manama, mji mkuu wa Bahrain na washiriki wa Jukwaa la Kimataifa la Uwekezaji kwa Wajasiriamali likiwa na wito wa pamoja na mambo mengine  likisihi jamii ya kimataifa na wadau wote katika sekta ya umma na binafsi kutumia nguvu ya ujasiriamali na uwekezaji katika nyanja zote za kiuchumi na kijamii kama kitovu cha kufanikisha Malengo ya Maendeleo Endelevu, SDGs kwa kupatia kipaumbele makundi maalum wakiwemo watu wenye ulemavu, wanawake, vijana na familia zinazohaha kutumia uwezo wa kuzalisha ili kujikimu kimaisha.

Baraza Kuu lilipitisha azimio mwaka 2012 lililoipa Palestina hadhi ya kuwa nchi isiyokuwa mwanachama katika Umoja wa Mataifa. (faili)
UN Photo/Rick Bajornas

Hadhi ya Palestina ndani ya UN yafafanuliwa 

Je, itachukua nini kwa Palestina kuwa Nchi Mwanachama kamili wa Umoja wa Mataifa? Wakati Baraza la Usalama linashughulikia suala hilo wakati vita vya uharibifu huko Gaza vikiingia mwezi wake wa saba, tuliangalia hali ya sasa ya Palestina na kile kinachohitajika kuwa Nchi Mwanachama wa Umoja wa Mataifa.

Mwanamke akiwa na mtoto wake mchanga akiwasikiliza wafanyakazi wa UNFPA katika kikao cha kuongeza uelewa kuhusu ukatili wa kijinsia katika Kituo cha One Stop katika Hospitali ya Sominé Dolo.
© UNFPA Mali/Amadou Maiga

Safari hatari na isiyo salama ya wajawazito nchini Mali

Aissata Touré, mwenye umri wa miaka 16, ndio kwanza amejifungua mtoto wake wa kwanza. Mama huyu ambaye naye ni mtoto, alikuwa na matumaini ya kjifungulia karibu na kijiji chao cha Ngouma nchini Mali, lakini mhudumu wa afya alimshauri aende hospitali kutokana na uwezekano wa kupata tatizo wakati wa kujifungua. Ilikuwa safari yenye changamoto na gharama kubwa.