Neno la Wiki- Chelewa
Wiki hii tunaangazia neno Keneka na mchambuzi wetu ni Onni Sigalla Mhariri Mwandamizi, katika Baraza la Kiswahili la Taifa, BAKITA, nchini Tanzania.
Kulingana na Bwana Sigalla neno hili lina maana zaidi ya moja, kwanza kama nomino, ala ya mziki ya kienyeji yenye vijiwa vinavotiwa katika mkebe, nyingine ni kuwa nyuma na wakati na chelewa nyingine kama nomino ni hali anayoiona mlevi baada ya kulewa jana, jina jingine ni maluweluwe.