Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Neno La Wiki

Neno la wiki: Hiba

Wiki hii tunaangazia neno "Hiba" na mchambuzi wetu ni Onni Sigalla, Mhariri Mwandamizi, katika Baraza la Kiswahili la Taifa, BAKITA, nchini Tanzania.

Bwana Sigalla anasema neno hiba lina maana mbili, moja ni kitu chochote anachopewa mtu kwa hiari au lengo la kuonyesha mapenzi, na lina maana sawa na idaya, adiya au azizi. Maana ya pili ni zawadi atoayo mtu kwa mpenzi au radhi ya mwenyezi Mungu kwetu.

Neno la wiki- Mchuuzi na Machinga

Katika neno la wiki hii leo tunaangazia maneno Mchuuzi na machinga. Mchambuzi wetu  ni Nuhu Zuberi Bakari, ambaye ni Naibu Mwenyekiti wa masuala ya mawasiliano kwenye Chama cha  Kiswahili cha Taifa nchini Kenya, CHAKITA

Bwana Zuberi anasema kwamba mchuuzi ni mtu anyeuza vitu vidogo vidogo alivyoweka sehemu iwe ni matunda, vichana au mboga alimradi anuza kwa bei ya reja reja. Machinga ni mtu yule yule anayeuza vitu vidogo vidogo lakini badala ya kuviuza katika sehemu anavibeba na kuzungusha iwe ni barabarani au kwingineko.

Neno la wiki- Mfasiri na Mkalimani

Wiki hii tunaangazia maneno Mfasiri na Mkalimani na mchambuzi wetu ni Onni Sigalla, Mhariri Mwandamizi, katika Baraza la Kiswahili la Taifa, BAKITA, nchini Tanzania.

Bwana Sigalla anasema mfasiri ni yule anayetafsiri neno au maneno kwa maandishi na mkalimani ni mtu anayeelezea kwa mdomo maneno yanayosemwa wakati ule ule kutoka lugha moja hadi nyingine .