Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Mashirikak ya UN na wadau wake wanatoa misaada kwa watu walioathiriwa na mapigano mapya huko Lviv
© UNOCHA/Allaham Musab

UN yazindua ombi la dola bilioni 4.2 kwa ajili ya kuwasaidia Waukraine

Takriban miaka miwili sasa tangu majeshi ya Urusi yaanzishe "vita kamili na kuikalia Ukraine, amesema leo mkuu wa Umoja wa Mataifa wa misaada ya kibinadamu na masuala ya dharura Martin Griffiths akitoa ombi la dharura la pamoja na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR la dola bilioni 4.2 ili kuwasaidia walio hatarini nchini Ukraine.

Malori yaliyosheheni msaada wa kibinadamu yakijiandaa kuingia Gaza kupitia kivuko cha Rafah
© UNICEF/Eyad El Baba

Mashirika ya UN yaomba kufunguliwe njia nyingine ya kufikisha misaada Gaza

Zikiwa ni zaidi ya siku 100 tangu kuibuka upya kwa mzozo huko Mashariki ya Kati, mashirika ya Umoja wa Mataifa hii leo yametoa taarifa inayoelezea kuongezeka kwa hatari ya baa la njaa na milipuko ya magonjwa ya kuambukiza huku yakisisitiza muarobaini pekee kwa sasa ni kuruhusu njia mpya za kuingiza misaada ya kwenda kutatua changamoto zinazowakabili wananchi walioko Gaza. 

Sauti
3'34"
Bi. Keita akizungumza na wanahabari huko Kalehe, Kivu Kusini.
MONUSCO/Michael Ali

MONUSCO yaafikiana na serikali ya DRC mikakati ya kuondoka nchini humo

Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC na Mkuu wa wa mpango wa Umoja wa Mataifa nchini humo MONUSC, Bi Bintou Keita na Naibu Waziri Mkuu, na Waziri wa Mambo ya nje Francophonie Christophe Lutundula walithibitisha jana Jumamosi Januari 13, dhamira ya vyombo hivyo viwili kufanya kazi kwa pamoja kwa mchakato wa kuondoka kwa MONUSCO nchini DRC kwa njia ya maendeleo, kuwajibika, heshima na kwa MONUSCO kuwa mfano wa kuigwa. 

Jamie McGoldrick mratibu mkazi wa muda na misaada ya kibinadamu katika eneo linalokaliwa la Palestina  akikutana na watu waliotawanywa kwenye eneo la Rafah Kusini mwa Gaza
OCHA /oPt

Msaada unaoingia Gaza hautoshelezi matakwa ya watu milioni 2.2: Jamie McGoldrick

Katika mahojiano maalum na UN News kupitia njia ya simu yaliyofanyika kutoka Jerusalem leo Januari 13 Jamie McGoldrick, Naibu Mratibu Maalum wa Muda na Mratibu Mkazi, wa Ofisi ya Mratibu Maalum wa Umoja wa Mataifa kwa ajili ya mchakato wa amani ya Mashariki ya Kati UNSCO, amesema, "kuna hali ya mshtuko na kiwango cha kukata tamaa. Na nadhani kuna hali ya kutokuwa na tumaini huko pia, kwa sababuwatu wa Gaza hawaoni hatua yoyote kwa kile wanachokikabili mbele yao.”