Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Dkt. Venance Shillingi, Mhadhiri Mwandamizi kutoka Chuo Kikuu Mzumbe nchini Tanzania akizungumza na Idhaa ya Umoja wa Mataifa kando mwa mkutano wa UN na wanazuoni uliofanyika New York, kuanzia Desemba 5-7 2023.
UN/Assumpta Massoi

Ni kwa vipi mfumo wa wamasai kujikwamua unaweza kuwa mfano kwa wengine Afrika?

Kitendo cha kabila la jamii ya wamasai kuweza kujimudu na maisha hata baada ya ukame uliosababishwa na mabadiliko ya tabianchi kuvuruga upatikanaji wa malisho kwa ajili ya mifugo yao kimeonekana kama moja ya mbinu mujarabu zinazoweza kusaidia nchi za Afrika kujengea mnepo wananchi wapo pindi mbinu walizozoea kujipatia kipato zinapovurugika.

Malori yaliyosheheni msaada wa kibinadamu yakijiandaa kuingia Gaza kupitia kivuko cha Rafah
© UNICEF/Eyad El Baba

Mashirika ya UN yaomba kufunguliwe njia nyingine ya kufikisha misaada Gaza

Zikiwa ni zaidi ya siku 100 tangu kuibuka upya kwa mzozo huko Mashariki ya Kati, mashirika ya Umoja wa Mataifa hii leo yametoa taarifa inayoelezea kuongezeka kwa hatari ya baa la njaa na milipuko ya magonjwa ya kuambukiza huku yakisisitiza muarobaini pekee kwa sasa ni kuruhusu njia mpya za kuingiza misaada ya kwenda kutatua changamoto zinazowakabili wananchi walioko Gaza. 

Sauti
3'34"
Watu waliojeruhiwa wakisubiri kutibiwa katika hospitali ya Al Shifa mjini Gaza. (Maktaba)
© WHO

Mzozo Gaza: Hospitali zazidi kuzidiwa uwezo, wagonjwa sakafuni

Ikiwa leo ni siku ya 93 tangu mapigano yaanze huko Ukanda wa Gaza kati ya jeshi la Israel na wanamgambo wa kipalestina waliojihami, likiwemo kundi la Hamas, mashirika ya Umoja wa Mataifa ya usaidizi wa kiutu yanazungumzia uwepo wa idadi kubwa ya vifo miongoni mwa wanawake na watoto huku yakisihi timu za madaktari ziruhusiwe kuingia eneo la Gaza ili ziendelee na jukumu la kuokoa maisha. 

Sauti
2'16"