Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Familia ambayo ilipoteza makazi yao kufuatia mafuriko akisafirisha mabaki vifaa vya nyumba yao kwa mtumbwi uliochimbwa kaskazini mwa Cameroon.
© UNHCR/Moise Amedje Peladai

Cameroon yatengewa dola milioni 6 kutoka CERF

Taarifa iliyotolewa na mfuko mkuu wa dharura wa Umoja wa Mataifa CERF mjini Yaounde, Cameroon, inaelezwa kuwa Mkuu wa masuala ya kibinadamu na misaada ya dharura wa Umoja wa Mataifa Martin Griffiths ameidhinisha kutengwa kwa Dola za Marekani milioni 6 kutoka katika mfuko huo ili kutoa msaada wa kuokoa maisha na ulinzi kwa watu walioathiriwa na majanga ya kibinadamu nchini Cameroon.

Uchunguzi wa virusi vya Ebola kwenye mpaka kati ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo , DRC na Uganda
WHO/Matt Taylor

Uganda yatangaza kutokomezwa kwa mlipuko wa Ebola

Uganda hii leo imetangaza kutokomeza mlipuko wa ugonjwa wa Ebola uliosababishwa na virusi aina ya Sudan, ikiwa ni chini ya miezi minne tangu kuthibitishwa kwa mgonjwa wa kwanza kwenye wilaya ya Mubende nchini humo 20 mwezi Septemba mwaka jana. Taarifa ya Thelma Mwadzaya inafafanua zaidi. 

 

Sauti
2'27"