Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

DR Congo

Clémence Ndabohweje, mwenye umri wa miaka 49, akisafisha vyombo nje ya makazi yake kwenye kambi ya wakimbizi ya ndani ya Kanyaruchinya huko Rutshuru jimboni Kivu Kaskazini nchini DRC kufuatia mashambulizi ya M23. Anaishi hapa yeye na watoto wake 6 na waj…
UNICEF/Arlette Bashizi

Hali DRC sasa imefikia pabaya, amani inahitajika haraka: UNICEF Chaiban

Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF anayehusika na shughuli za kibinadamu na operesheni za Ugavi, Ted Chaiban, amehitimisha ziara ya siku tano mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, ambako alikutana na mamlaka na kujionea athari mbaya za kuongezeka kwa migogoro kwa watu walio hatarini, haswa wanawake na watoto.

Watu waliokimbia makazi yao kutokana na migogoro wanaishi katika kambi ya muda karibu na Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
© WFP/Benjamin Anguandia

DRC: Mashambulizi Goma yaua raia 12, UN yalaani

Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, Bintou Keita amelaani vikali shambulio la leo la mabomu dhidi ya makazi mawili ya kuhifadhi wakimbizi wa ndani huko Lac-Vert na Mugunga takribani kilometa 13 hadi 15 kutoka Goma mji mkuu wa jimbo la Kivu Kaskazini.

Francine na watoto wake watatu walilazimika kuondoka kijijini kwake kutokana na mzozo usiokoma mashariki mwa DRC. Sasa wanapokea msaada wa WFP katika kambi ya wakimbizi wa ndani huko Kivu Kaskazini.
© WFP/Michael Castofas

WFP DRC waomba msaada wa $Mil 425 kusaidia wakimbizi wa ndani

Wakati Mashariki mwa nchi ya Jamhuri ya Kidemorkasia Kongo DRC ikiripoti kuwa na zaidi ya wakimbizi wa ndani 738,000 kwa kipindi cha mwaka huu wa 2024 pekee kutokana na kuongezeka kwa machafuko, Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani WFP limeeleza kuwa na uhitaji wa haraka wa dola milioni 425 ili waweze kuwasaidia wakimbizi hao wanaoongezeka kila uchao. 

Sauti
1'49"