Hali DRC sasa imefikia pabaya, amani inahitajika haraka: UNICEF Chaiban
Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF anayehusika na shughuli za kibinadamu na operesheni za Ugavi, Ted Chaiban, amehitimisha ziara ya siku tano mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, ambako alikutana na mamlaka na kujionea athari mbaya za kuongezeka kwa migogoro kwa watu walio hatarini, haswa wanawake na watoto.