Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

DR Congo

Askari wa mpango wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani MONUSCO nchini Congo DRC akilinda wakati helkopta ya WFP ikiwasilisha msaada kwenye kambi ya wakimbizi wa ndani Ituri
© UNICEF/Diana Zeyneb Alhindawi

UDADAVUZI: Nyenzo tano zinazohitajika kudumisha amani

Mwaka 1948, Umoja wa Mataifa ulichukua hatua muhimu kwa kupeleka askari wa kulinda amani kusaidia nchi katika safari yao ya kuelekea amani. Tangu wakati huo, zaidi ya watu milioni mbili wanajeshi, polisi na raia wamehudumu katika operesheni zaidi ya 70 za kulinda amani duniani kote, wakitoa msaada huku kukiwa na migogoro inayoendelea au matokeo ya migogoro hiyo.

Clémence Ndabohweje, mwenye umri wa miaka 49, akisafisha vyombo nje ya makazi yake kwenye kambi ya wakimbizi ya ndani ya Kanyaruchinya huko Rutshuru jimboni Kivu Kaskazini nchini DRC kufuatia mashambulizi ya M23. Anaishi hapa yeye na watoto wake 6 na waj…
UNICEF/Arlette Bashizi

Hali DRC sasa imefikia pabaya, amani inahitajika haraka: UNICEF Chaiban

Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF anayehusika na shughuli za kibinadamu na operesheni za Ugavi, Ted Chaiban, amehitimisha ziara ya siku tano mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, ambako alikutana na mamlaka na kujionea athari mbaya za kuongezeka kwa migogoro kwa watu walio hatarini, haswa wanawake na watoto.

Watu waliokimbia makazi yao kutokana na migogoro wanaishi katika kambi ya muda karibu na Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
© WFP/Benjamin Anguandia

DRC: Mashambulizi Goma yaua raia 12, UN yalaani

Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, Bintou Keita amelaani vikali shambulio la leo la mabomu dhidi ya makazi mawili ya kuhifadhi wakimbizi wa ndani huko Lac-Vert na Mugunga takribani kilometa 13 hadi 15 kutoka Goma mji mkuu wa jimbo la Kivu Kaskazini.