Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Makala Maalum

Csaba Kőrösi  Rais wa UNGA77 akiendesha mjadala wa wazi wa Baraza Kuu katika siku ya mwisho ya mjadala huo
UN Photo/Cia Pak

Körösi, akunja jamvi la mjadala wa ngazi ya juu wa UNGA77

Magari yaliyotanda kuzunguka makao makuu ya Umoja wa Mataifa kwa ajili ya kuhakikisha usalama wakati wa wiki ya mjadala wa ngazi ya juu wa viongozi kwenye Baraza Kuu UNGA77 sasa yameondoka na barabara iliyofungwa kufunguliwa, polisi wengi na maafisa wa ujasusi ambao walizuia njia za kuelekea kwenye jengo la Umoja wa Mataifa, nao wametrejea kwenye majukumu yao ya kila siku, kilomita za vyuma vilivyokuwa vizuizi kuzunguka eneo hilo la Umoja wa Mataifa New York, vinavyojulikana kama Turtle Bay navyo vimesafirishwa kwa malori hadi kwenye maghala kusubiri hadi mwakani kwani wiki ya mjadala wa ngazi ya juu imemalizika kwenye Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa  .

Kambi ya wakimbizi ya Za'atari nchini Jordan inayoonekana kutoka juu ina wakimbizi kutoka Syria.
UN Photo/Mark Garten)

Watoto wangu wananiuliza Syria ni nini? Kambi ya Zaatar ikiingia muongo mwingine

Mwaka 2022 ni  miaka 10 tangu kuanzishwa kwa kambi ya wakimbizi ya Za’atari nchini Jordan, kambi ambayo inasimamiwa na Umoja wa Mataifa. Ni kambi kubwa zaidi Mashariki ya Kati na moja ya kambi kubwa zaidi duniani ikiwa ni maskani ya wasyria 80,000. UN News au Habari za UN imezungumza na baadhi ya wakimbizi kuhusu maisha katika kambi hiyo, na matumaini yao kwa siku zijazo. 

Rahot akiwa na mjukuu wake, Hassan, kijijini ambako alihamia karibu na kituo cha lishe kinachoendeshwa na SCI na kufadhiliwa na SHF.
Sara Awad – Save the Children

Napanda milima kuhakikisha mjukuu wangu anapata tiba ya Utapiamlo

Kila siku asubuhi na mapema kukipambazuka na jua kuchomoza Rahot mwenye umri wa miaka 55 huamka na kumbeba mgongoni mjukuu wake Hassan tayari kwakuaza safari ya takriban kilometa 20 yenye vilima kwenda kituo cha kumpatia lishe mjukuu huyo ili kuokoa maisha yake kutokana na kuwa na utapiamlo mkali.