Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Makala Maalum

Watalaam, hudumu za kiafya wakati wa ujauzito na kujifungua zinaweza kuzuia Fistula.
© UNFPA Mozambique

Mambo 5 unayopaswa kufahamu kuhusu Fistula: UNFPA 

Fistula itokanayo na uzazi ni nini? 

Ni jeraha kubwa la wakati wa kujifungua ambalo humpokonya mwanamke au msichana afya yake, haki na utu.  

Ni shimo linalotokea kati ya njia ya uzazi na kibofu ambayo husababisha kutoweza kudhibitiwa kwa mkojo.  

Pia ni shimo kati ya njia ya uzazi na njia ya haja kubwa husababisha kinyesi kuvuja bila kujizuia.

Judith Candiru, Muuguzi Msaidizi katika kituo cha afya cha Midigo, wilaya ya Yumbe nchini Uganda.
© UNICEF/Zahara Abdul

Hawavumi ila wamo; mashujaa wa COVID-19 

Kwa baadhi ya watu, huhisi ni kazi. Kwa wengine ni wajibu. Na kuna wale wanaona ni muhimu. Miaka miwili iliyopita, shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni, WHO lilitangaza mlipuko wa ugonjwa wa Corona au COVID-19 kuwa janga duniani. Hakuna yeyote aliyetambua kinachofuatia. Lakini katika kipindi cha miezi 24 baada ya tangazo hilo, watu wa kipekee, wanawake kwa wanaume wameibuka na kunusuru jamii zao. Majina yao hayafahamiki, lakini vitendo vya mashujaa hawa bila shaka yoyote ile, vimefanya dunia kuwa pahala salama na bora. Je ni akina nani?