Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Makala Maalum

Mtoto mwenye ulemavu wa ngozi tena mwenye ulemavu wa kutoona akisoma kwa kupitia maandishi maalum ua nukta nundu kwa watu wasioona au wenye uoni hafifu
© UNICEF/Pirozzi

Utafiti na Ushahidi juu ya Watoto wenye Ulemavu: UNICEF

Ingawa Malengo ya Maendeleo Endelevu yanahimiza kuwa hakuna mtoto anayepaswa kuachwa nyuma. Lakini utafiti uliofanywa na Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumiwa watototo UNICEF unaonesha kuwa kati ya watoto milioni 240 wenye ulemavu duniani, nusu hawajawahi kuhudhuria shule, takriban theluthi moja hawapati chakula bora na chakutosha na pia watoto wenye ulemavu wanawakilishwa kwa njia isiyo sawa na wengi wao wanaachwa nyuma.