Elimu sio ufunguo wa maisha tu ni msingi wa maendeleo:UN
Elimu ni nguzo muhimu katika jamii na ndio ufunguo wa maisha. Ili kuleta usawa katika jamii, juhudi nyingi zimeongezwa kasi ili bidhaa hiyo iwafikie watoto na vijana wa jinsia zote mbili kwa mujibu wa ripoti ya karibuni iliyotolewa na mashirika ya Umoja wa Mataifa japo imetoa angalizo kwamba maeneo ya vijijini bado yamesalia nyuma hata baada ya harakati kuimarishwa.