Simulizi ya Hussein Juma Hassan: Kufeli masomo si kufeli maishani
Nilipopata fursa ya kusoma ili nipate cheti cha kutambuliwa rasmi kuwa mchomeleaji vyuma mwenye stadi, sikuchelea bali nilikuwa na hamu ya kuchukua fursa hiyo. Awali sikuwa na uthibitisho wa stadi hiyo na uzoefu niliokuwa nao ulitokana na kufanya kazi hii kwa miaka 25 na kujifunza nikiwa kazini. Ni simulizi ya Hussein Juma Hassan kutoka Zanzibar, Tanzania, baba wa familia ya mke na watoto 6.