Siyo ulemavu wote unaonekana-Wataalam wa Afya
Huku ulimwengu ukiadhimisha siku ya kimataifa ya walemavu na kauli mbiu ya mwaka huu ikiwa “sio ulemavu wote unaonekana” ni bayana kuwa watu wengi duniani wanaishi na ulemavu wa aina fulani ambao hauonekani ambao wakati mwingine unaweza kuchukuliwa kuwa labda tabia zao na hata watu hao kukumbwa na unyanyapaa katika jamii. Mara nyingi ulemavu unaozingatiwa huwa ule unaonekana kwa mfano ulemavu wa miguu, mikono au macho ingawa nao bado wanakumbana na changamoto nyingi.