Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Makala

National Institute of Allergy and Infectious Diseases, NIH, US

Kenya kuhakikisha kuna miakakati endapo Virusi vya Corona vitazuka:WHO

Shirika la afya ulimwenguni WHO jana Alhamisi limetangaza kuwa virusi vipya vya corona ni dharura ya afya ya kimataifa inayotia wasiwasi likizitaka nchi zote kuchukua tahadhari na kujiandaa endapo virusi hivyo vitazuka katika nchi zao. Kwa sasa virusi hivyo kitovu chake kimekuwa mji wa Wuhan nchini China ambako Kwa mujibu wa WHO jumla ya visa 9692 vimethibitishwa katika majimbo 31, na kati ya hivyo watu 1239 wako katika hali mbaya, 213 wamefariki dunia na wagonjwa 103 wametibiwa, kupona na kuruhusiwa kwenda nyumbani. Na nje ya China kuna visa 68 vilivyothibitishwa katika nchi 18.

Sauti
5'41"
UNEP GRID Arendal/Peter Prokosch

Kumbukumbu na mikakati ya kupambana na nzige, Uganda

Wakati shirika la chakula na kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) limeonya juu ya janga la njaa katika ukanda wa Africa Mashariki  na pembe ya Afrika kutokana na uvamizi wa nzige nchini Ethiopia, Somalia na Kenya. Nchini Uganda hofu inazidi kutanda wakati ambapo nzige hao waperipotiwa kuvamia maeneo ya mpaka wake na Kenya, na kuharibu mazao ya kilimo na mimea katika mamilioni ya ekari. FAO imeitahadharisha Uganda na Sudan Kusini kuwa makini na kuchukua hatua ili kukabiliana na wimbi hilo la nzige endapo litazuka.

Sauti
3'48"
© UNICEF/Naftalin

Tunawaondoa wasichana wanaojiuza katika shughuli hiyo na kuwafundisha ujasiriamali- Carol Evelyn Nzogere

Moja ya azma ya jumla ya kufanikisha Malengo ya Maendeleo Endelevu yaani SDGs ni kuhakikisha hakuna anayebaki nyuma bila kujali hali yake katika jamii. Shirika lisilo la kiserikali la Christ’s Daughters mjini Mwanza Tanzania chini ya Uongozi wa Carol Evelyn Nzogere wanawatafuta na kuwashawishi wasichana wadogo wanaojihusisha na biashara ya ukahaba ili kuwabadilisha na kuwaelimisha kuhusu ujasiriamali kwa lengo la kuwainua kiuchumi na kuokoa afya zao.

Sauti
4'11"
UN News/Patrick Newman

Lengo letu ni kuhakikisha kwamba wanawake na wasichana wanaonekana kidijitali-Sambuli

Kwa miaka mingi, wanawake walikuwa wakiachwa nyuma katika maendeleo na hata maswala ya kijamii ikichochewa na utamaduni na mitazamo dume kwenye jamii. Kwa kutambua hilo Umoja wa Mataifa kupitia lengo namba tano la malengo ya maendeleo endelevu linalenga kuziba pengo hilo ambalo kwa miaka limebinya haki za wanawake na wasichana. Moja ya maeneo ambako mwanamke ameachwa nyuma ni ulimwengu wa dijitali na kwa kutambua hilo Katibu Mkuu aliunda jopo maalum kwa ajili ya kusongesha malengo hayo mbele.

Sauti
3'39"
UN Environment/Hannah McNeish

Mabadiliko ya tabianchi yametuathiri sana watoa tiba za asili- Mugisha John

Wakati tukiwa tumeingia katika muongo wa ukamilishaji wa malengo 17 ya maendeleo endelevu, dunia inahaha kupambana na mabadiliko ya tabianchi ambayo yanaiweka sayari dunia katika hatari ya kukumbwa na majanga mbalimbali. Uharibifu wa mazingira si tu unaathiri moja kwa moja hali ya hewa kama vile ukame, upepo mkali na majanga mengine, pia kupitia makala hii iliyoandaliwa na Tumaini Anatory wa redio washirika Karagwe FM ya mkoani Kagera, mtaalamu wa tiba asilia Mugisha John wa Kayanga Karagwe anaeleza namna mabadiliko ya tabianchi yalivyoathiri kazi yao ya utafutaji wa tiba za mitishamba.

Sauti
3'26"
World Bank / Sarah Farhat

Tanzania imepiga hatua katika kuhakikisha kila mtoto anaandikishwa shuleni japo changamoto zipo

Stella Vuzo wa UNIC Dar es Salaam anamuhoji Ayubu Kafyulilo mtaalamu katika shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF nchini Tanzania anayesimamia masuala ya ujifunzaji na elimu kwa ajili ya vijana na watoto ambao wako katika mazingira magumu na walio nje ya shule. Kwanza anaanza kwa kueleza hali ya elimu ikoje nchini humo baada ya kuanza kwa mfumo wa elimu bila malipo kwa ngazi ya kuanzia elimu ya awali, msingi hadi kidato cha nne.

Sauti
6'37"
UN News

Ninasisitiza sana vijana kuchukua fursa zilizopo sasa, bila kusubiri- Professa Nyoni

Ujumuishaji wa vijana katika ngazi za maamuzi na za kimaendeleo ni suala ambalo linasisitizwa kila uchao. Lakini maandalizi ya vijana hao katika nafasi mablimbali yanafanyika shuleni na pia kwenye vyuo vikuu. Mmoja wa watoa elimu ambao wanasaidia vijana sio tu kutambua uwepo wa fursa lakini pia kutumia fursa hizo ni Professa Nyoni ambaye kwa kutambua nafasi finyu zilizopo anahimiza vijana kuchukua fursa zilizopo sasa. 

Sauti
3'17"
World Bank/Arne Hoel

Vijana na mikakati ya kuepuka changamoto ya ukosefu wa ajira, Uganda

Katika zama hizo ambazo ulimwengu unakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa ajira kwa watu wengi, zipo sababu nyingi zinazochangia uwezekano wa kijana kupata fursa ya ufadhili wa elimu au kuajiriwa ili kuepuka changamoto za kutokuwa na ujuzi unaoendana na soko la ajira.  Sababu hizo ni pamoja na tabia au mienendo ya kijana husika katika jamii na malengo ya kijana binafsi. Nchini Uganda, ukosefu wa ujuzi unaoendana na kazi zilizopo ni miongoni mwa changamoto kubwa ambazo serikali na wadau wake wa mafuta wamekuwa wakishughulikia kwa karibu muongo mmoja uliopita.

Sauti
4'
UNnewskiswahili/Patrick Newman

Ibua Afrika ni daraja kati ya wanawake na wawekezaji nchini Kenya- Mumbi Ndung'u

Wakati dunia ikihaha kutumiza malengo ya maendeleo endelevu ya Umoja wa Mataifa, nchi na watu binafsi wanaibuka na njia bunifu kwa ajili ya kusongesha malengo hayo mbele kuelekea ukomo wake mwaka 2030. Moja wa watu ambao wamebuni njia mpya za kuwezesha makundi katika jamii ikiwemo wanawake na vijana na Mumbi Ndung'u mwanzilishi wa shirika la Ibua Afrika ambayo ilichipukia kwenye mitandao ya kijamii lakini sasa ikitumia jukwa mbali mbali kuwakutanisha wawekezaji na wadau wengine na vijana na wanawake kwa ajili ya kuendeleza jamii.

Sauti
3'45"
UN News/ John Kibego

Nyasi vamizi zageuka fursa kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi nchini Uganda

Mabadiliko ya tabianchi yanazidi kusababisha wasiwasi miongoni mwa jamii za wafugaji Afrika na kwingineko ulimwenguni hasa kutokana ukame wa muda mrefu. Hata hivyo, nchini Uganda hatua zinachukuliwa ambapo wameanza kubaini nyasi zinazoweza kuhiili mabadiliko haya ya tabianchi na hatimaye kuzihamishia katika maeneo mbalimbali ya nchi ili ziwasaidie badala ya kutegemea malisho asilia katika eneo fulani.

Mmoja wa wale ambao wamevalia suala hilo njuga ni Mbunge wa Kaunti ya Butemba wilaya ya Kyankwanzi Innocent Pentagon Kamusiime ambaye amepanda nyasi aina ya  Kikuyu.

Sauti
3'42"