Majanga duniani ni matokeo ya kushindwa kuchagua jambo sahihi la kufanya - Guterres
Mapigano, umaskini, ukosefu wa usawa, mivutano ya kijiografia na kisiasa, na janga la tabianchi ni matokeo ya kile ambacho dunia inachagua kufanya au inashindwa kuchagua kufanya, amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres hii leo huko Kampala nchini Uganda.