Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Eva Ghamaharo, mkazi wa Kaunti ya  Mto Tana, mnufaika wa mradi wa dharura wa mgao wa fedha kwa manusura wa mafuriko unaotekelezwa na UNICEF Kenya.
UNICEF/James Ekwam

Mafuriko Kenya: Mgao wa fedha waleta matumaini kwa wakazi wa Kaunti ya Mto Tana- UNICEF

Wingu kubwa la mvua likiwa limetanda kwenye mji wa Garsen, ulioko kaunti ya Mto Tana nchini Kenya, Eva Ghamaharo, mama wa watoto watatu anarejea nyumbani akitembea na watoto wake wawili mapacha wenye umri wa miaka mitatu baada ya kununua matumizi ya nyumbani kutoka kioski cha jirani. Watoto hawa wawili mapacha wa kike ni Grace na Jane na wanaonekana na furaha kwani angalau leo mama yao ameweza kuwanunulia kila mmoja pakiti ya maziwa na wanakunywa kwa furaha.

Sauti
2'6"
Olle Mjengwa mshiriki wa Jukwaa la Vijana 2030, la Baraza la Kiuchumi na Kijamii la Umoja wa Mataifa, ECOSOC, akizungumza na Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa kandoni mwa mkutano huo uliofanyika kwa siku tatu, New York ,Marekani.
UN/Assumpta Massoi

UNDP yashindanisha vijana kusaka majawabu kwa tabianchi , washindi kupata kitita cha fedha

Vijana wameelezwa kuwa na umuhimu mkubwa katika kusongesha mbele moja ya ajenda kubwa za 2030 za Umoja wa Mataifa ambayo ni kukabiliana na janga la mabadiliko ya tabianchi. Na katika kutambua mchango wao Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa maendeleo UNDP, limekuja na mbinu mbalimbali za kuwashirikisha vijana ili wasiachwe nyuma katika suala hilo na mengine kama ya kuleta amani na usalama. Olle Mjengwa anayefanyakazi ya UNDP ofisi ya Roma Italia amezungumza na UN News kandoni mwa Jukwaa la vijana la Baraza la Kiuchumi na Kijamii ECOSOC lililokunja jamvi mwishoni mwa wiki ili kufafanua kuhusu ushirikishwaji huo wa vijana katika UNDP