Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Katibu Mkuu  António Guterres ametembelea maonesho ya picha ya "Mikononi mwao: Wanawake wachukua umiliko wa amani" katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa
UN Photo/Mark Garten)

Muda wa kurudisha nyuma saa ya haki za wanawake umepita, sasa iende mbele- Guterres alieleza Baraza

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa leo limekuwa na mjadala wa wazi kuhusu wanawake, amani na usalama ambapo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema wakati umefika kwa baraza hilo kuonesha kwa vitendo uungaji wake mkono wa harakati za wanawake katika ujenzi na uendelezaji wa amani badala ya kusalia maneno matupu.  Flora Nducha na maelezo zaidi.

Sauti
3'18"
Katika kituo cha ukusanyaji wa pamba Brazil ambako pamba hutenganishwa na mbegu kabla haijashindiliwa na kuhifadhiwa
FAO/Alberto Conti

Pamba, kitambaa kinachositiri  zaidi ya familia milioni 100 duniani:UN

 Leo ni siku ya pamba duniani ikiwa ni maadhimisho ya kwanza kabisa ya siku hiyo kuenzi zao ambalo kitabaa chake kinatengeneza mavazi ya kila siku yaliyosheheni kwenye mkabati mengi ya nguo na ni kitambaa kizuri, rahisi kuvaa, kukitunza na kinadumu kwa muda mrefu. Lakini kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa thamani ya pamba ni zaidi ya kitambaa kama inavyofafanua taarifa ya Flora Nducha 

Sauti
2'40"