Kampuni Uganda zaitikia wito wa UN za hatua kwa tabianchi
Nchini Uganda katika mji wa Hoima, kampuni moja imechukua hatua ya kutekeleza wito wa Umoja wa Mataifa wa kuchukua hatua kwa tabianchi kwa kuondokana na taka za plastiki zinazoharibu mazingira kwa kuzirejeleza katika njia ambayo siyo tu inasafisha mazingira bali pia inaleta kipato kwa waajiriwa wakiwemo wanawake na vijana.