Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari Mpya

Ujenzi wa madarasa nchini Mozambique yanayohimili hali mbaya za hewa ikiwemo vimbunga vinavyong’oa mapaa.
UN Habitat Mozambique

Iwe mvua iwe upepo mkali madarasa yetu ni salama: Mwanafunzi Msumbiji

Kila mwaka, Msumbiji hukabiliwa na matukio ya hali mbaya za hewa kupindukia kama vile vimbunga na mafuriko, matukio ambayo husababisha uharibifu wa shule na hatimaye watoto kushindwa kujifunza. Hata hivyo, ujenzi wa madarasa yanayohimili matukio kama vile pepo kali na mafuriko umeleta nuru na matumiani kwa watoto, wazazi na walimu. Madarasa haya yanawezesha watoto kubakia salama hata wakati wa mvua na upepo mkali. Hali hii ni uwekezaji wa kudumu kwani ni  hakikisho kwa watoto kuendelea kupata elimu na mustakabali wao kuwa bora. 

Sauti
4'11"
Mahakama ya Kimataifa ya Haki ikisikiliza kessi ya Afrika Kusini dhidi ya Israel mjini The Hague. (Maktaba)
ICJ-CIJ/ Frank van Beek

ICJ yaitaka Israeli iepushe mauaji ya kimbari Gaza

Mahakama ya Kimataifa ya Haki, ICJ hii leo imeamua kuwa Israel lazima ichukue hatua zote za kuzuia vitendo vya mauaji ya kimbari katika mashambulizi yake dhidi ya wapalestina huko, Gaza, uamuzi unaofuatia shauri lililowasilishwa na Afrika Kusini la kutaka Mahakama hiyo ya Umoja wa Mataifa ichukue hatua za awali kwa mujibu wa Mkataba wa kimataifa wa kuepusha mauaji ya kimbari wa mwaka 1948. 

Sauti
2'13"
Sukhdev Vishwakarma na binti yake Meenu wote wakiwa ni wakulima wanatu,mia maji ya kisima cha kupampu na sola katika shamba la Gurinder Singh lenye ukubwa wa ekari 80 Jagadhri.
© CCAFS/Prashanth Vishwanathan

Kuna nishati safi na fedha katika kinachoonekana kuwa ni takataka – FAO

Kilimo ni moja ya shughuli za kibinadamu zinazochangia katika uchafuzi wa hewa. Kwa kulitambua hilo, FAO kote ulimwenguni inachagiza kile inachokiita kwa lugha ya kiingereza Bioeconomy yaani uchumi ambao msingi wake unatokana na matumizi ya rasilimali za kibayolojia zinazopatikana kwenye mazingira; kwa mfano kurejesha taka katika uzalishaji wa nishati safi, mbadala wa mafuta ya kisukuku. Kupitia harakati hizo, FAO inasaidia wakulima kuongeza mapato, kupunguza uzalishaji wa hewa chafuzi na kuchangia kupunguza taka ulimwenguni kwa kubadilisha mifumo ya zamani ya kilimo ambayo ilikuwa inachangia kuharibu mazingira.

 

Sauti
1'42"
Makazi ya wakimbizi ya Kyangwali yaliyoko wilaya ya Kikuube magharibi mwa Uganda.
UN News

Makazi ya wakimbizi Uganda yatumia elimu kusongesha amani miongoni mwa wakimbizi

Nchini Uganda katika makazi ya wakimbizi ya Kyangwali wilaya ya Kikuube magharibi mwa taifa hilo, suala la mchango wa elimu kwenye amani liko dhahiri kwani tulipotembelea katika makazi hayo, Yahya Kato ambaye ni Mwalimu Mkuu katika Shule ya msingi Kasonga kwenye makazi hayo ya wakimbizi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC na Sudan anazungumzia kile wanachofanya. 

Sauti
1'15"
Wanafunzi katika shule moja ya msingi mashariki mwa Nigeria wakisubiri mwalimu aingie masomo yaanze.
© UNICEF/Mackenzie Knowles-Cour

Siku ya Kimataifa ya Elimu 2024 yatumika kukabiliana na kauli za chuki

Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) limeyatumia maadhimisho ya mwaka huu ya Siku ya Kimataifa ya Elimu kuangazia jukumu muhimu la elimu na walimu katika kukabiliana na kauli za chuki, jambo ambalo limekithiri katika miaka ya hivi karibuni kutokana na matumizi ya mitandao ya kijamii na hivyo kuharibu muundo wa jamii kote duniani. 

Sauti
2'10"