Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Makala Maalum

Didas Byaruhanga, mwenye umri wa miaka 64 anayeishi na VVU na kisukari nchini Uganda.
WHO

Kisukari ni moja ya muuaji mkubwa kwa wenye VVU Uganda: WHO

Jijini Kampala, nchini Uganda, zaidi ya watu milioni 1.4 wanaishi na virusi vya ukimwi  VVU na kati ya hao, asilimia 5.8 wana ugonjwa wa kisukari. Ugonjwa wa kisukari ni kawaida miongoni mwa watu wanaoishi na virusi vya ukimwi na ni mojawapo ya sababu kuu za vifo miongoni mwa watu hao kwa mujibu wa shirika la afya la Umoja wa Mataifa duniani WHO. 

Katika muda wa wiki mbili tu, Wapalestina wengi huko Gaza wamepoteza kila kitu nyumba zao, wanafamilia na hali yoyote ya kawaida, wakiwa wamebanwa kwenye vibanda vya kujihifadhi, vyenye chakula na maji kidogo na hakuna umeme, hawajui nini kitatokea siku …
UNDP PAPP/Abed Zagout

Simulizi kutoka Gaza: “Ninatafuta mtandao ili kuangalia maeneo yaliyoathirika huku nikitumai sitaona jina la mume wangu wala familia yangu kwenye orodha”

Hebu vuta tasirwa, mama akiwabembeleza watoto wake usiku, hofu ya kutengana nao ikija kama kivuli, kujaribu awezavyo kujilinda yeye na familia yake, ili ‘wasiwe kumbukumbu’ hata hivyo, hadithi yetu ni kumbukumbu tu sasa, lakini wakati ujao bado haujaandikwa, nikiamka kesho, nataka hili limalizike, ilinirejee mahali patakatifu, kwenye nyumba yetu. 

Lori likiwa limejaa chupa za maji ya kunywa  likielekea Al Arish mji ulio kilometa 32 kusini mwa mpaka wa Gaza
© UNICEF/Mohamed Ragaa

Udadavuzi: Kuna nini ndani ya msafara wa misaada kwenye kivuko cha Gaza

Chini ya kilomita moja kutoka Gaza, vibao vya kuengeshean chakula, mafuta, maji, na dawa ni miongoni mwa mamia ya tani za misaada ya kuokoa maisha iliyopakiwa kwenye msafara mrefu wa malori yakiwa yamesimama kwenye upande wa Misri wa kivuko cha mpakani ch a Rafah, huku madereva wakisubiri ruksa ya Israel ili waweze kufikia Wapalestina milioni 2.3 waliozingirwa na walionaswa katika mzozo wa vita vinavyoendelea.