Simulizi: Sijawahi kuona vita kama hii, hii ni Nakba kwa Wapalestina
Watu wa Gaza wanakabiliwa na “mshtuko mkubwa” kutokana na mzozo unaoendelea baina yao na Israel, kwa mujibu wa mfanyakazi wa Umoja wa Mataifa anayefanya kazi katika eneo hilo.
Watu wa Gaza wanakabiliwa na “mshtuko mkubwa” kutokana na mzozo unaoendelea baina yao na Israel, kwa mujibu wa mfanyakazi wa Umoja wa Mataifa anayefanya kazi katika eneo hilo.
Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya Watu na Afya ya Uzazi, UNFPA nchini Sudan Mohamed Lemine, amesema shirika hilo limeweka mashine mpya ya kusagisha unga kwa wanakijiji wa Shanisha, katika jimbo la Blue Nile, nchini Sudan ili kuwapunguzia adha wananchi wa eneo hilo.
Katika nyakati za zamani, wakulima walikuwa wakiangalia anga la usiku ili kujua wakati sahihi wa kupanda au kuvuna, katika zama za sasa taarifa hizo hazipatikani tena kutoka kwenye kuangalia nyota, bali kutoka kwenye unajimu unaotengenezwa na wanadamu kwa kutumia programu za simu.
Jijini Kampala, nchini Uganda, zaidi ya watu milioni 1.4 wanaishi na virusi vya ukimwi VVU na kati ya hao, asilimia 5.8 wana ugonjwa wa kisukari. Ugonjwa wa kisukari ni kawaida miongoni mwa watu wanaoishi na virusi vya ukimwi na ni mojawapo ya sababu kuu za vifo miongoni mwa watu hao kwa mujibu wa shirika la afya la Umoja wa Mataifa duniani WHO.
Hali mbaya inayowakabili mamia kwa maelfu ya Wapalestina huko Gaza inaweza kuwa mbaya zaidi, kutokana na uhaba mkubwa wa mafuta ambao unatishia kusimamisha chakula na shughuli zingine za kibinadamu.
Hebu vuta tasirwa, mama akiwabembeleza watoto wake usiku, hofu ya kutengana nao ikija kama kivuli, kujaribu awezavyo kujilinda yeye na familia yake, ili ‘wasiwe kumbukumbu’ hata hivyo, hadithi yetu ni kumbukumbu tu sasa, lakini wakati ujao bado haujaandikwa, nikiamka kesho, nataka hili limalizike, ilinirejee mahali patakatifu, kwenye nyumba yetu.
Miaka 23 baada ya makubaliano muhimu ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa yanayoangazia wanawake, amani na usalama, wanawake na wasichana bado wanabeba mzigo mkubwa wa migogoro na wanabaki na uwakilishi mdogo katika maamuzi yanayohusu mahitaji ya na haki zao.
Akili mnemba imebadili fani ya sanaa na utamaduni kwa njia ambazo ha ikutarajiwa. Hata hivyo mabadiliko hayo ni ya muda mrefu.
Chini ya kilomita moja kutoka Gaza, vibao vya kuengeshean chakula, mafuta, maji, na dawa ni miongoni mwa mamia ya tani za misaada ya kuokoa maisha iliyopakiwa kwenye msafara mrefu wa malori yakiwa yamesimama kwenye upande wa Misri wa kivuko cha mpakani ch a Rafah, huku madereva wakisubiri ruksa ya Israel ili waweze kufikia Wapalestina milioni 2.3 waliozingirwa na walionaswa katika mzozo wa vita vinavyoendelea.
Ni alfajiri na mapema jua likichomoza kisiwani Pemba, pwani ya Tanzania. Baadhi ya wakazi wa kisiwa hiki tayari wako kwenye mitumbwi wanaelekea kuvuna mazao yao.