Suluhu ya Somalia ni kutekeleza muafaka wa kisiasa na kufanya uchaguzi:Mahiga
Somalia ambayo kwa zaidi ya miongo miwili sasa haina serikali kuu inazidi kujikuta katika njia panda ya kisiasa kwa mgawanyiko kughubika uhusiano baina ya Rais wa serikali ya mpito na spika wa bunge.
Kwa mujibu wa mwakilishi maalumu wa Umoja wa Mataifa Somalia balozi Agustine Mahiga tofauti hizo zinazidisha adha kwa mamilioni ya wasomali waliochoka vita na wenye kiu ya amani ya kudumu.