Ulemavu sio kulemaa tunachotaka ni kujumuishwa: Mbunge Mollel
Siku hii ya kimataifa ya watu wenye ulemavu inapoadhimishwa kote duniani watu wenye ulemavu wamekuwa wakipaza sauti zao kila kona kwamba ulemavu sio kulemaa wanachohitaji ni ujumuishwashi na miundombinu Rafiki itakayowawezesha kushiriki katika kusongesha mbele ajenda ya maendeleo endelevu kama wengine.
Miongoni mwa watu hao ni mbunge Amina Mollel kutoka nchini Tanzania, yeye mwenyewe ni mlemavu na anawakilisha watu wenye ulemavu wa taifa hilo bungeni, akizungumza nami kwa njia ya simu kutoka mjini Arusha amesisitiza nafasi ya wenye ulemavu katika ujumbe wake.
Mila na desturi Kilimanjaro bado ni kikwazo cha haki ya mwanamke:Minde
Mila na desturi zimeendelea kuwa mtihani mkumu katika juhudi za ukombozi wa mwanamke katika kupata haki na sheria sehemu mbalimbali duniani ikiwemo mkoani Kilimanjaro nchini Tanzania, kwa nini?