Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mahojiano

Mpatanishi anapofungasha virago ni mashaka- Dkt. Salim

Hatma ya amani Mashariki ya Kati hususan kati ya wapalestina na waisraeli imeingia dosari baada ya Marekani kutangaza kutambua Yerusalem kama mji mkuu wa Israel. Marekani ikichukua msimamo huo nchi 128 wanachama wa  wa Umoja wa Mataifa wamepitisha azimio la kuitaka nchi hiyo ibadili uamuzi huo, uamuzi ambao unaenda mbali zaidi na kuhamisha ubalozi wa Marekani kutoka mji mkuu wa sasa wa Israel, Tel Aviv kwenda Jerusalem. Lakini nini maana ya hatua hizi? Flora Nducha amezungumza na Dkt.

Ufugaji nyuki sasa ni mtaji dhidi ya umaskini huko Kyela, Tanzania

Kupitia lengo namba moja la kutokomeza umasikini lililomo kwenye ajenda ya  maendeleo endelevu ya Umoja wa Mataifa  ya mwaka 2030, serikali zinahimizwa kutafuta mbinu mbadala kuwawezesha wananchi kupitia miradi mbalimbali ili kujikwamua na umasikini ifikikapo mwaka 2030.

Tanzania ni nchini mojawapo ambako serikali imechukua jukumu la kutoa elimu ya SDGs kwa kutafsiri malengo yao endelevu kwa lugha ya kiswahili ili kutoa mwongozo kwa wananchi na pili kuwapatia fursa za ujasiriamali kupitia miradi  mbalimbali kama  ufugaji, uvuvi, kilimo na kadhalika.

Vijana Somalia badilisheni simulizi potofu kuhusu vijana

Nchini Somalia wiki hii wamezindua sera ya taifa ya vijana ambayo kwayo inazungumzia hatua za kukwamua vijana kuelekea utekelezaji wa malengo ya maendeleo endelevu, SDGs. Uzinduzi huo umefanyika wakati wa mkutano wa taifa wa vijana kwenye mji mkuu Mogadishu ukihudhuria na viongozi wa kitaifa na kimataifa. Miongoni mwao ni mjumbe maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu vijana Bi. Jayathma Wickramanayake  ambaye amewasihi vijana sasa kushika usukani ili kubadili simulizi potofu ya kwamba kijana ni lazima atatumbukia kwenye misimamo mikali na kuleta ghasia.

(Picha:UN/Aliza Eliazarov)

Tumesikitishwa na kushtushwa na shambulio dhidhi ya walinda amani wetu:Mahiga

Tumeshtushwa sana na kusikitishwa na shambulio la jana dhidi ya walinda amani wetu. Amesema hayo waziri wa Mambo ya nje na ushirikiano wa Afrika ya Mashariki wa Tanzania Balozi Augustine Mahiga alipozungumza leo na Flora Nducha wa idhaa hii kufuatia kuuawa kwa walinda amani wa Tanzania 14, wengine 38 kujeruhiwa wakiwemo walio hali mahtuti na wanne kutojulikana walipo huko Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo DRC, baada ya kundi la waasi wa ADF kuzamia kituo cha walinda amani hao.

(MAHOJIANO KATI YA FLORA NDUCHA NA BALOZI AUGUSTINE MAHIGA)

Utokomezaji ukatili kwa wanawake sio jukumu la wanawake pekee bali jamii nzima: UM

Vita ya kupinga  ukatili dhidi ya wanawake katika mifumo yote ni moja vipaumbele katika  ajenda ya Umoja wa mataifa ya  maendeleo ya mwaka 2030.

Juma hili likiwa ni la maadhimisho ya siku yakutokomeza ukatili dhidi ya wanawake duniani itakayofikia kilele chake kesho  tarhe 25 Novemba ,  mashirika mbalimbali ya Umoja wa Mataifa pamoja na asasi za kiraia walijumuika kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa new York Marekani kuunga mkono agenda vita hivyo.

Tanzania tunaelekea kulinda amani CAR na Sudan Kusini- Dkt. Mwinyi

Mkutano wa masuala ya operesheni za ulinzi wa amani za Umoja wa Mataifa umekunja huko Vancouver, Canada kwa lengo la kuangazia jinsi ya kuboresha operesheni hizo. Idadi kubwa ya operesheni ziko barani Afrika ambako mizozo na vita imegubika eneo hilo. Miongoni mwa washiriki alikuwa Waziri wa ulinzi na jeshi la kujenga taifa kutoka Tanzania Dkt. Hussein Mwinyi. Kando mkutano huo Mathew Wells wa Idhaa ya Umoja wa Matafa alizungumza naye katika mahojiano haya ambayo maswali yataletwa kwako na Flora Nducha. Kwanza Dkt.

Kutoka Tanzania hadi Sudan Kusini kusaidia ulinzi wa raia- Meja Paschal

Maafisa wa jeshi la wananchi wa Tanzania, JWTZ ni miongoni mwa watendaji katika ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani huko Sudan  Kusini, UNMISS. Maafisa hao wana majukumu mbalimbali yote yakichangia kufanikisha ulinzi wa raia na amani kwenye taifa hilo change zaidi duniani ambalo sasa limegubikwa na vita vya wenyewe kwa wenyewe tangu mwezi disemba mwaka 2013. Je ni yapi miongoni mwa majukumu hayo?

Hali ya mjane kutoka Uganda ni msumari wa moto juu ya kidonda-sehemu 1

Wakati Umoja wa Mataifa ukichagiza nchi kuhakikisha kwamba hakuna mtu anayeachwa nyuma kuelekea ukomo wa malengo ya maendelo endelevu yaani SDGs bado kuna changamoto ambazo huenda zikakwamisha ufikiaji wa malengo hayo. Wanawake na waisichana mara kwa mara wanakabiliwa na aina mbali mbali ya ubaguzi ikiwemo suala la urithi wa mali hususan katika jamii zilizoko nchi zinazoendelea.

Ubunifu wa nguo za magome ya miti na uhifadhi wa mazingira Burundi-sehemu 1

Katika  Juhudi za kuunda ajira na  kuhifadhi mazingira, msichana kutoka Burundi Annick Kabatesi ameanzisha mradi wa kutengeneza nguo zitokanazo na magome ya miti.  Nguo hizo zimetajwa kuwa zinazingatia uhifadhi wa mazingira. Bi. Kabatesi ambaye ni mwanamitindo pia amejijengea umaarufu mkubwa kwa  kutengeneza nguo hizo za magome ya miti  baada ya nguo hizo kuwavutia viongozi wakuu Serikalini.

Tuangazie yanayotuweka pamoja badala ya migawanyiko- Ruteere

Katika zama za sasa, siasa zinaghubikwa na mwelekeo wa baadhi ya vyama kujipatia umaarufu kupitia ajenda za kibaguzi kutoka kwa wafuasi wao. Umoja wa Mataifa kupitia ofisi yake ya haki za binadamu imekuwa ikipaza sauti kupinga mwelekeo huo ukisema kuwa ni ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu. Hoja hiyo na nyingine nyingi ni miongoni mwa mambo ambayo Joseph Msami amezungumza na mtaalamu huru wa Umoja wa Mataifa kuhusu ubaguzi wa zama za sasa Mutuma Ruteere ambaye amekamilisha jukumu lake tarehe 31 mwezi wa Oktoba mwaka huu wa 2017.