Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Mvulana anakimbia katika mitaa iliyoharibiwa ya Gaza.
© UNRWA/Ashraf Amra

GAZA: Miezi 6 ya mzozo Guterres akemea matumizi ya Akili Mnemba

Kesho kutwa jumapili ikiwa ndio itatimu miezi sita ya mzozo wa Gaza, huko Mashariki ya Kati, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres hii leo amezungumza na waandishi wa habari jijini New York, Marekani akirejelea wito wake wa sitisho la mapigano kwa misinigi ya kiutu, kuachiliwa kwa mateka wote bila masharti, ulinzi wa raia na misaada ya kiutu ifikie walengwa bila vikwazo vyovyote huku akikgusia pia Israeli kutumia akili mnemba kwenye operesheni zake. 

Sauti
2'40"
Mfanyakazi wa UNMAS akichunguza mabomu ya kutegwa ardhini, jimbo la Equatoria kati, Sudan Kusini.
© UN Photo/Isaac Billy

Mtu 1 huuawa kila saa kwa bomu au kilipuzi - UN

Mabomu, vilipuzi na vifaa vingine vya mlipuko vinaendelea kuua na kujeruhi watu katika maeneo mengi yenye changamoto kubwa za migogoro duniani na matokeo yake vifaa hivyo vya mlipuko, kwa wastani hukatili Maisha ya mtu mmoja kila saa, na waathirika wakubwa wakiwa ni watoto kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa.

Ufunguzi wa kituo cha malezi ya watoto wachanga huko Kajiado nchini Kenya ili kuwezesha mama zao kurudi shule.
UN News

Wadau nchini Kenya waitikia wito wa Umoja wa Mataifa wa kumwezesha mtoto wa kike

Mkutano wa 68 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake duniani, CSW68 ulifunga pazia hivi majuzi jijini New York Marekani ukipigia chepuo uwekezaji kwa wanawake na wasichana, na leo tunabisha hodi nchini Kenya wasichana waliokumbwa na ujauzito utotoni na kukatishwa ndoto za kuendelea na masomo au kupata ajira wamepata jawabu la changamoto wanazokumbana nazo pindi wakijifungua watoto wao. 

Sauti
7'35"
Katikati ya mji wa Port-au-Prince Haiti machafuko yamesababisha kundi kubwa la watu kutawanywa
© UNICEF/Herold Joseph

Hatua za kijasiri zinahitajika ili kutokomeza mateso na ukatili Haiti – UN

Ufisadi, ukwepaji sheria na ukosefu wa utawala bora uliogubikwa na viwango vya juu vya uhalifu unaofanywa na magenge, vimemomonyoa utawala wa kisheria nchini Haiti na kudhoofisha taasisi za serikali ambazo zinakaribia kusambaratika, imesema ripoti mpya ya Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Binadamu iliyochapishwa hii leo huku ikitaka hatua za haraka na za kijasiri zichukuliwe ili kukabiliana na hali ya janga inayokumba taifa hilo la Karibea.

Ceodou Mandingo 'Babuu wa Kitaa' (aliyevaa kofia), Mtetezi wa watu wenye Down Syndrome.
Ceodou Mandingo (Babuu wa Kitaa)

Watoto wenye Down syndrome wana uwezo wakipewa nafasi - Ceodou Mandingo 'Babuu wa Kitaa'

Hii leo katika kuadhimisha siku ya kimataifa ya kuhamasisha kuhusu ugonjwa unaothiri uwezo wa mtu kujifunza au Down syndrome tutamsikia Ceodou Mandingo almaarufu Babuu wa Kitaa wa nchini Tanzania ambaye ni mzazi mwenye mtoto aliye na changamoto hiyo na ameikubali hali ya mwanaye na anajitahidi kuelimisha umma kuhusu ugonjwa huo. Kumbuka kuwa mwezi Desemba mwaka 2011, Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kupitia azimio namba (A/RES/66/149) lilitangaza Machi 21 kuwa Siku ya Kimataifa ya Down Syndrome. Maadhimisho ya kwanza yalianza mwaka uliofuata.  

Kamanda wa TANZBATT-10, Luteni Kanali John Peter Kalabaka akimkabidhi bendera ya Tanzania Luteni Kanali  Vedasto Ernest Kikoti ikiwa ni ishara ya kukabidhiana majukumu ya ulinzi wa amani huko Beni Mavivi jimboni Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokra…
TANZBATT-10

Wananchi DRC eleweni na ikubalini dhamira ya UN ya kulinda raia - TANZBATT-11

Hii leo huko jimboni Kivu Kaskazini mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, kikosi cha 10 cha Tanzania (TANZBATT-10)  kilichoko kwenye brigedi ya mapigano (FIB) ya ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, MONUSCO imekabidhi majukumu kwa kikosi cha 11, TANZBATT-11, katika hafla iliyofanyika eneo la Beni-Mavivi. Msimulizi wetu ni Kapteni Abubakari Muna, Afisa Habari wa TANZBATT-10.

Sauti
3'28"