Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Makala

UN News/Stella Vuzo

Tanzania inashikamana na ulimwengu kusongesha ajenda ya mazingira: Waziri Jafo

Mkutanowa Umoja wa Mataifa wa Baraza la mazingira duniani UNEA6 leo umekunja jamvi jijini Nairobi Kenya baada ya kukutanisha wadau zaidi ya 7000, kutoka nnyanja mbalimbali kwa lengo la kukabiliana na changamoto kubwa tatu zinazoikabili dunia ambazo ni mabadiliko ya tabianchi, upotevu wa bayoanuai na uchafuzi wa mazingira. Viongozi mbalimbali wanaowakilisha nchi zote wanachama wa Umoja wa Mataifa wamepata fursa ya kuwasilisha taarifa zao na kushiriki katika mjadiliano.

Sauti
4'38"
Stella Vuzo/UNIS Nairobi

Vijana tukipewa nafasi tuna mchango wa kulinda mazingira: UNEA6

Wakati jijini Nairobi Kenya mkutanowa Umoja wa Mataifa wa Baraza la mazingira duniani UNEA6 ukielekea ukingoni leo ikiwa ni siku yake ya 4, vijana wanaoshiriki mkutano huo wamepaza sauti zai na kusistiza kuwa wakipewa nafasi basi wana mchango mkubwa katika vita dhidi ya uharibifu wa mazingira na kusongesha mbele ajenda ya maendeleo endelevu SDGs.  Leo mkutanoni huko Stella Vuzo afisa habari wa kitengo cha habari cha Umoja wa Mataifa jijini Nairobi UNIS amezungumza na vijana wawili wanaoshiriki mkutano huo ambao ni wanaharakati wa mazingira wanaotumia sayansi na sanaa kuleta mabadiliko

Sauti
3'49"
© UNICEF

UNICEF Rwanda: Je wajua  kwamba watoto Rwanda wanaanza kupokea chanjo zao za kawaida karibu na nyumbani?

Katika makala tunaangazia chanjo kwa watoto nchini Rwanda ambako Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF linaifadhili Rwanda Biomedical Centre (RBC) ambalo ni shirika kuu la kitaifa la utekelezaji wa afya lenye jukumu la kufanya utafiti wa kisayansi, kutoa huduma za uchunguzi, na kutekeleza afua za kiafya ili kulinda taifa la Rwanda dhidi ya magonjwa na matishio mengine ya kiafya. Anold Kayanda anasimulia.

Sauti
3'33"
UN Photo/Elma Okic

Umoja wa Mataifa sio tatizo – Rais wa Baraza Kuu

Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa Dennis Francis Pamoja na mambo mengine amesema Umoja wa Mataifa "sio tatizo" bali tatizo linatokana na kwamba baadhi ya nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa wanahisi wanaweza kukiuka mkataba wa Umoja wa Mataifa watakavyo na kukiuka sheria za kimataifa bila kuadhibiwa. Anold Kayanda anaeleza zaidi.

Sauti
4'41"
UNIS/Nairobi

Wanawake ili tufanikiwe lazima tujitume: Dkt. Elizabeth Kimani

Mkutano wa wanawake katika nyanja ya diplomasia umefanyika wiki hii katika Chuo Kikuu cha Nairobi nchini Kenya. Viongozi wa ofisi za Umoja wa Mataifa jijini Nairobi na Geneva Uswisi wamewasilisha mada mbele ya umati wa watu waliohudhuria mkutano huo wakiwemo Mabalozi wastaafu na wanaotumikia nchi zao hivi sasa nchini Kenya kuhusu nafasi ya Mwanamke katika ddiplomasia na katika kutimiza malengo ya maendeleo endelevu SDGs. Dkt.

Sauti
2'59"
UN News/Ziad Taleb

Huku wanakimbia vita wanawake wa Gaza inakuwaje wakiwa katika hedhi?

Kunapozuka mizozo na machafuko wananchi wote wanaathirika kwasababu maisha yao yanaparanganyika kabisa tofauti na walivyokuwa wamezoea. Watoto waliokuwa wakienda shule sasa hawaendi, si wafanyabiashara, wakulima wala viongozi wa dini wanaotekeleza majukumu yao ya kila siku na suala moja lililo kweli kwa kila mtu ni kuwa wanatafuta kila namna ya kuokoa maisha yao na wengi njia hiyo huwa ni kukusanya virango vyao kidogo wanavyoweza kubeba na kukimbia kuokoa nafsi zao. 

Sauti
4'35"
Redio Domus/Kevin Keitany

Redio ni chombo cha mawasiliano kilicho rafiki

Licha ya redio ambacho ni chombo cha kuaminiwa kwa miaka mingi katika usambazaji wa taarifa, kukabiliwa na changamoto nyingi katika nyakati hizi ambazo kuna utitiri wa teknolojia za usambazaji wa habari, bado inaonekana watu wana imani kubwa na chombo hiki kwa sababu mbalimbali. Wachache kati ya wengi, ni wadau hawa tuliozungumza kutoka Afrika Mashariki. Kwanza ni Rose Haji, mwanahabari mwandamizi wa siku nyingi nchini Tanzania akieleza kuhusu kazi kuu za redio.

Sauti
3'28"
© WFP/Eulalia Berlanga

Benki ya Maendeleo ya Afrika na UNHCR waungana kusaidia wakimbizi nchini Sudan Kusini

Vita vinapotokea wananchi wanalazimika kusaka kila namna ya kujilinda na kuokoa maisha yao. Mambo yanapokuwa mabaya watu hao hulazimika kuacha kila kitu nyuma na kukimbia kwenda kusaka hifadhi sehemu nyingine. Watu hao wanapoondoka wanaondoka na ujuzi wao mfano kama alikuwa muuguzi, mfanya biashara, fundi muashi au taaluma yoyote ile. 

Mara nyingi sehemu wanazofikia wakimbizi hao iwe ndani au nje ya nchi zao hujikuta wakipata mahitaji muhimu kwa ajili ya kuishi kama vile chakula cha msaada na matibabu, kiufupi watu hawa hugeuka kuwa tegemezi. 

Sauti
3'47"