Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Wanawake ili tufanikiwe lazima tujitume: Dkt. Elizabeth Kimani

Wanawake ili tufanikiwe lazima tujitume: Dkt. Elizabeth Kimani

Pakua

Mkutano wa wanawake katika nyanja ya diplomasia umefanyika wiki hii katika Chuo Kikuu cha Nairobi nchini Kenya. Viongozi wa ofisi za Umoja wa Mataifa jijini Nairobi na Geneva Uswisi wamewasilisha mada mbele ya umati wa watu waliohudhuria mkutano huo wakiwemo Mabalozi wastaafu na wanaotumikia nchi zao hivi sasa nchini Kenya kuhusu nafasi ya Mwanamke katika ddiplomasia na katika kutimiza malengo ya maendeleo endelevu SDGs. Dkt. Elizabeth Kimani Murage anayefanyakazi na kituo cha utafiti na idadi ya watu Afrika (African population and research center) kama mtafiri mkuu ni miongoni mwa waliohudhuria mkutano huo na amezungumza na Stella Vuzo afisa habari wa kitengo cha habari cha Umoja wa Mataifa Nairobi UNIS katika makala hii na anaanza kwa kumueleza kwanini aliona ni muhimu kuhudhuria mkutano huo.

Audio Credit
Anold Kayanda/Flora Nducha
Audio Duration
2'59"
Photo Credit
UNIS/Nairobi