Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Makala

UN News/ Jonatha Joram

Ninarejeleza bidhaa chakavu ili kusafisha mazingira na kuokoa viumbe hai-Jonatha Joram

Ikiwa imesalia takribani miaka kumi kufikia mwaka 2030 ambao umepangwa kuwa mwaka ambao malengo 17 ya maendeleo endelevu, SDGs yatakuwa yametimizwa. Juhudi kote duniani zinaendelea kuhakikisha lengo hilo linafikiwa. Nchini Tanzania, msichana mbunifu Jonatha Joram anayeishi katika jiji la Dar es Salaam ameamua kushiriki katika utunzaji wa mazingira kwa kurejeleza bidhaa ambazo tayari zimetumika ili ziweze kutumika tena badala ya kutupwa na kuchafua mazingira. Katika mahojiano haya na Anold Kayanda wa UN News, Jonatha anaanza kwa kueleza anavyozifanya shughuli zake

Sauti
3'37"
UN-Habitat/Julius Mwelu

Wanawake wapigania nafasi katika sekta ya mafuta, Turkana Kenya

Katika eno la Turkana nchini Kenya shughuli za uchimbaji wa mafuta zimeshika kasi, lakini kama ilivyo sehemu nyingi duniani kuna baadhi ya kazi ikiwemo ya uchimbaji mafuta zimekuwa zikichukuliwa kama ni kazi za wanaume. Lakini kwa wanawake wa Turkana wanasema hapana , kila kazi inaweza kufanywa na kila mtu endapo fursa inatolewa na jitihada zinafanyika. Na  matakwa ya wanawake hao ni kuweza kushiriki katika sekta hiyo yenye manufaa kwani uhusisha uwekezaji wa mabilioni ya dola za kimarekani.

Sauti
4'7"