Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Mtoto akipita kwenye mitaa ya jimbo la Khan Younis huku majengo yakiwa yamesambaratishwa kwa makombora. Jimbo hili liko kusini mwa Ukanda wa Gaza.
© UNICEF/Eyad El Baba

GAZA: Tangu vita ianze makombora ya Israel yamepiga moja kwa moja shule 212

Mashambulizi makubwa yanayofanywa na Israeli dhidi ya Gaza kufuatia mashambulizi ya kigaidi yaliyofanywa na wanamgambo wa kipalestina wa Hamas dhidi ya taifa hilo yamejumuisha makombora yaliyorushwa moja kwa moja dhidi ya shule 212  kwenye eneo hilo lililozingirwa, umeonesha uchambuzi mpya uliofanywa kwa pamoja kati ya Umoja wa Mataifa na wadau wake.

Innoss B(kushoto) na Mkurugenzi wa WFP DRC, Peter Musoko(Kulia). Innoss B akitia saini barua rasmi ya kuteuliwa kama Msaidizi wa Ngazi ya Juu wa WFP nchini DRC, akihimiza milo yenye afya na lishe bora.
© WFP/Charly Kasereka

Innoss’B kutumia muziki kusongesha elimu na lishe bora DRC

Nimeshuhudia njaa mara nyingi sana wakati wa utoto wangu, kabla ya kwenda shule tulikuwa na njaa na kabla ya kulala tulikuwa na njaa, ndivyo asemavyo mwanamuziki Innocent Balume, al maaruf Innoss’B ambaye ametangazwa kuwa muungaji mkono wa ngazi ya juu wa shirika la  Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula duniani, WFP katika kusongesha milo yenye afya na lishe bora nchini mwake Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

Sauti
2'6"
Mtoto kutoka Mtedera Zambia akipweza chanjo ya kipindupindu.
Picha ya Gavi Alliance/Duncan Graham-Rowe

WHO Zambia, yashirikiana na Serikali kutokomeza Kipindupindu

Juhudi na ushirikiano wa pamoja wa wahudumu wa afya, vituo na Jamii, vimefanikisha kukomesha mlipuko wa kipindupindu uliozuka nchini Zambia kwa mujibu wa Shirika Umoja wa Mataifa la Afya Duniani WHO nchini Zambia, ambalo limeeleza kwamba ugunduzi wa mapema na matibabu husaidia kukabiliana na ugonjwa huo na kupunguza matukio na vifo.

Sauti
2'9"