Guterres atambua uamuzi wa ICJ kuhusu Gaza, sasa kuwasilisha notisi Baraza la Usalama
Muda mfupi baada ya Mahakama ya Kimataifa ya Haki, ICJ huko The Hague, Uholanzi kupitisha uamuzi wa kuitaka Israel pamoja na mambo mengine ichukue hatua zote chini ya uwezo wake wote ku kuepusha mauaji ya kimbari dhidi ya wapalestina huko Ukanda wa Gaza na kuhakikisha misaada ya kiutu inaingia, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametambua uamuzi huo.