Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Msichana mwenye umri wa miaka 11 ameketi kwenye vifusi vya nyumba huko Rafah, kusini mwa Ukanda wa Gaza.
© UNICEF/Eyad El Baba

Guterres atambua uamuzi wa ICJ kuhusu Gaza, sasa kuwasilisha notisi Baraza la Usalama

Muda mfupi baada ya Mahakama ya Kimataifa ya Haki, ICJ huko The Hague, Uholanzi kupitisha uamuzi wa kuitaka Israel pamoja na mambo mengine ichukue hatua zote chini ya uwezo wake wote ku kuepusha mauaji ya kimbari dhidi ya wapalestina huko Ukanda wa Gaza na kuhakikisha misaada ya kiutu inaingia, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametambua uamuzi huo. 

Naibu Mkurugenzi Mkuu wa IOM, Amy Pope, (mwenye skafu ya buluu) akizungumza na wanawake wa Somalia wakati wa ziara yake ya siku  nne nchini humo.
IOM

Hali ya kutisha ya zaidi ya watu milioni 10 waliokimbia makazi yao kutokana na mizozo nchini Sudan isipuuzwe - IOM

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji, IOM Amy Pope amesema hali ya kutisha inayokumba zaidi ya watu milioni 10 waliofurushwa kwenye makazi  yao nchini Sudan kutokana na mapigano haipaswi kupuuzwa. Taarifa ya IOM iliyotolewa leo Geneva, Uswisi na Port Sudan nchini Sudan imemnukuu akieleza kwamba watu milioni 10.7 sasa wamekimbia makazi yao kutokana na migogoro nchini Sudan, na kati yao hao, milioni tisa wamo  ndani ya nchi hiyo kulingana na takwimu mpya kutoka IOM. 

Sala na muda wa ukimya katika Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Kumbukumbu ya Umoja wa Mataifa ya Kuwakumbuka Wahanga wa Mauaji ya Holocaust.
UN Photo/Manuel Elías

Mauaji ya mangamizi: Hakuna jamii iliyo salama dhidi ya ubaguzi

Kuelekeea siku ya kumbukumbu ya waliofariki katika mauaji ya maangamizi makubwa au Holocaust dhidi ya wayahudi hapo kesho 27 Januari Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amekumbusha kuwa mauaji hayo yaliyoanza mwaka 1941- 1945 yalitanguliwa na maelfu ya miaka ya ubaguzi, watu kufukuzwa, kuhamishwa na kuangamizwa na kwamba vitendo kama hivyo sasa vinaenea ulimwenguni. 

Mahakama ya Kimataifa ya Haki ikisikiliza kessi ya Afrika Kusini dhidi ya Israel mjini The Hague. (Maktaba)
ICJ-CIJ/ Frank van Beek

ICJ yaitaka Israeli iepushe mauaji ya kimbari Gaza

Mahakama ya Kimataifa ya Haki, ICJ hii leo imeamua kuwa Israel lazima ichukue hatua zote za kuzuia vitendo vya mauaji ya kimbari katika mashambulizi yake dhidi ya wapalestina huko, Gaza, uamuzi unaofuatia shauri lililowasilishwa na Afrika Kusini la kutaka Mahakama hiyo ya Umoja wa Mataifa ichukue hatua za awali kwa mujibu wa Mkataba wa kimataifa wa kuepusha mauaji ya kimbari wa mwaka 1948. 

Sauti
2'13"
Sukhdev Vishwakarma na binti yake Meenu wote wakiwa ni wakulima wanatu,mia maji ya kisima cha kupampu na sola katika shamba la Gurinder Singh lenye ukubwa wa ekari 80 Jagadhri.
© CCAFS/Prashanth Vishwanathan

Kuna nishati safi na fedha katika kinachoonekana kuwa ni takataka – FAO

Kilimo ni moja ya shughuli za kibinadamu zinazochangia katika uchafuzi wa hewa. Kwa kulitambua hilo, FAO kote ulimwenguni inachagiza kile inachokiita kwa lugha ya kiingereza Bioeconomy yaani uchumi ambao msingi wake unatokana na matumizi ya rasilimali za kibayolojia zinazopatikana kwenye mazingira; kwa mfano kurejesha taka katika uzalishaji wa nishati safi, mbadala wa mafuta ya kisukuku. Kupitia harakati hizo, FAO inasaidia wakulima kuongeza mapato, kupunguza uzalishaji wa hewa chafuzi na kuchangia kupunguza taka ulimwenguni kwa kubadilisha mifumo ya zamani ya kilimo ambayo ilikuwa inachangia kuharibu mazingira.

 

Sauti
1'42"