Gaza: Wakati watu wakiendelea kukimbia Rafah UN yahimiza kufunguliwa upya kwa njia za misaada
Bila dalili ya kusitisha operesheni ya kijeshi ya Israel katika mji wa kusini mwa Gaza wa Rafah leo Ijumaa, wahudumu wa kibinadamu wa Umoja wa Mataifa wametoa wito mpya wa kusitishwa kwa mapigano kama "tumaini pekee la kuepusha umwagaji damu zaidi na kurejesha misaada inayohitajika kuliko wakati mwingine wowote”.