Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Utoaji wa chanjo dhidi ya COVID-19 nchini Kenya.
WHO Video

Kenya yaanza kutoa chanjo dhidi ya COVID-19 

Serikali ya Kenya inaendelea na kampeni ya chanjo dhidi ya corona au COVID-19 baada ya shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF kupata na kusafirisha dozi zaidi ya milioni moja hadi Nairobi kupitia mkakati wa kimataifa wa upatikanaji wa chanjo COVAX. 

 

Sauti
2'43"
Katibu Mkuu Antonio Guterres akihudhuria kuoneshwa wazi kwa 'Darasa la Janga' katika Makao Makuu ya UN ili kuangazia hitaji la serikali kuweka kipaumbele kufungua shule.
UN Photo/Eskinder Debebe)

Watoto milioni 168 wamepoteza mwaka 1 wa masomo, hilo nalo ni janga - Guterres 

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres hiI leo Machi 2 ametembelea eneo katika moja ya viwanja vya Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa mjini New York Marekani, ambalo limetumiwa na shirika la kuhudumia watoto la Umoja wa Mataifa UNICEF, kutoa wito kuhusu dharura ya elimu iliyotokana na COVID-19 na kukuza ufahamu kuhusu uhitaji wa serikali kuzifungua shule. 

Walinda amani wa Umoja wa Mataifa kutoka Tanzania wanaohudumu MONUSCO nchini DRC wakizungumza na wananchi wakazi wa jimbo la Kivu Kaskazini.
TANZBATT_8/Kapteni Tumaini Bagambo.

TANZBATT_7 yafunga virago DRC na kukabidhi kijiti kwa TANZBATT_8

Kikosi cha 7 cha Tanzania, TANZBATT_7 kwenye kikosi maalum cha kujibu mashambulizi, FIB cha ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, MONUSCO kimetamatisha jukumu lake rasmi na kukabidhi bendera kwa kikosi cha 8 au TANZBATT_8. Shuhuda wetu kutoka Beni, jimboni Kivu Kaskazini ni Luteni Issa Mwakalambo, afisa habari wa TANZBATT_7. 

Sauti
3'19"