Baraza Kuu lakutana kumuenzi Hayati Magufuli
Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa leo limekuwa na kikao rasmi cha kumuenzi na kumkumbuka Rais wa 5 wa Tanzania Dkt. John Magufuli aliyefariki dunia tarehe 17 mwezi uliopita.
Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa leo limekuwa na kikao rasmi cha kumuenzi na kumkumbuka Rais wa 5 wa Tanzania Dkt. John Magufuli aliyefariki dunia tarehe 17 mwezi uliopita.
Ikiwa kesho Aprili 14 ni siku ya ugonjwa wa Chagas, shirika la kimataifa la kufanikisha uwepo wa tiba nafuu duniani, Unitaid linaloratibiwa na shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO, limesema uwepo wa Covid-19 umefanya hali kuwa mbaya zaidi kwa hali ambayo tayari ilikuwa mbaya kutokana na ugonjwa wa Chagas.
Kikao cha 65 cha kamisheni ya hali ya wanawake duniani CSW65 leo kimefungua pazia mjini New York Marekani kikishirikisha wadau kutoka kila pembe ya dunia ambao safari hii kwa asilimia kubwa wanashirikia kupitia mtandaoni kwa sababu ya athari na vikwazo vya janga la corona au COVID-19.
Serikali ya Kenya inaendelea na kampeni ya chanjo dhidi ya corona au COVID-19 baada ya shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF kupata na kusafirisha dozi zaidi ya milioni moja hadi Nairobi kupitia mkakati wa kimataifa wa upatikanaji wa chanjo COVAX.
Hii leo ikiwa ni siku ya wanawake duniani, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema janga la COVID-19 limefuta maendeleo ya miongo kuelekea usawa wa jinsia huku wanawake wakikumbwa zaidi na machungu, bado kundi hilo limesalia kuwa mstari wa mbele kwenye hatua dhidi ya janga la Corona.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres hiI leo Machi 2 ametembelea eneo katika moja ya viwanja vya Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa mjini New York Marekani, ambalo limetumiwa na shirika la kuhudumia watoto la Umoja wa Mataifa UNICEF, kutoa wito kuhusu dharura ya elimu iliyotokana na COVID-19 na kukuza ufahamu kuhusu uhitaji wa serikali kuzifungua shule.
Umoja wa Mataifa umeelezea masikitiko yake kufuatia matokeo ya ahadi zilizotolewa katika mkutano wa kimataifa wa kuchangisha fedha kwa ajili ya kusaidia Yemen mwaka huu wa 2021 ambayo inakabiliwa na janga la kibinadamu, linalotajwa kuwa kubwa zaidi duniani. Makisio yalikuwa dola bilioni 3.85 lakini iliyopatikana ni takribani dola bilioni 1.7.
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa leo limekuwa na mjadala kuhusu vitisho vya amani na usalama duniani visababishwavyo na janga la tabianchi ambapo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema janga la tabianchi ni changamoto ya ushirikiano wa kimataifa katika zama za sasa.
Kikosi cha 7 cha Tanzania, TANZBATT_7 kwenye kikosi maalum cha kujibu mashambulizi, FIB cha ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, MONUSCO kimetamatisha jukumu lake rasmi na kukabidhi bendera kwa kikosi cha 8 au TANZBATT_8. Shuhuda wetu kutoka Beni, jimboni Kivu Kaskazini ni Luteni Issa Mwakalambo, afisa habari wa TANZBATT_7.
Ngozi Okonjo-Iweala kutoka Nigeria amechaguliwa kuwa Mkurugenzi Mkuu wa shirika la biashara duniani, WTO.