Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari Mpya

Wasichana wakiwa darasani katika Kituo cha Kujifunza cha Kasi katika Mkoa wa Wardak katika mkoa wa kati wa Afghanistan.
© UNICEF/Christine Nesbitt

UN yasema wasichana wa Afghanistan kuzuiwa kuhudhuria Chuo Kikuu ni pigo jingine la kikatili kwa haki za wanawake na wasichana

Umoja wa Mataifa umetaka mamlaka za watalibani nchini Afghanistani kubadili uamuzi wake wa kuzuia wasichana kujiunga na elimu ya Vyuo Vikuu nchini humo, tangazo ambalo limetolewa na taifa hilo la barani Asia Jumanne wiki hii ikiwa ni miezi tisa tangu watangaze kuzuia wasichana kuendelea na elimu ya sekondari.

 

Sauti
2'2"
CBD umepitisha makubaliano ya kihistoria yaliyofikiwa katika mkutano huo kuhusu mpango mpya wa kuhifadhi na kulinda asili kwa kutumia Mfumo mpya wa Kimataifa wa Bayonuai, (GBF).
Picha: UN Biodiversity

Jumuiya ya kimataifa na wadau wa mazingira wakaribisha Mfumo mpya wa Kimataifa wa Bayonuai (GBF)

Ikiwa leo ni tamati ya mkutano wa 15 wa nchi wanachama wa mkataba wa kimataifa kuhusu bayonuai, COP15, huko Montréal, Canada, wadau mbalimbali wa mazingira wamekaribisha makubaliano ya kihistoria yaliyofikiwa katika mkutano huo kuhusu mpango mpya wa kuhifadhi na kulinda asili kwa kutumia Mfumo mpya wa Kimataifa wa Bayonuai, (GBF).

Sauti
1'54"
Jengo la dawati la jinsia na watoto kwa ajili ya kupinga na kutokomeza ukatili wa kijinsia na mila kandamizi dhidi ya wanawake na wasichana
Picha: UNFPA/Warren Bright

UNFPA Tanzania yakabidhi msaada wa dawati la jinsia wilayani Simanjiro

Shirika la Umoja wa Mataifa la idadi ya watu duniani na masuala ya afya ya uzazi UNFPA nchini Tanzania limekabidhi jeshi la polisi mkoani Manyara msaada wa jengo la dawati la jinsia na watoto ikiwa njia moja wapo ya jitihada za kupinga na kutokomeza ukatili wa kijinsia na mila kandamizi dhidi ya wanawake, wasichana na watoto.

Sauti
4'59"