Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Ukraine

Leo ni Siku ya uhuru wa Ukraine hapa ni mjini Kyiv
© UNDP Ukraine/Krepkih Andrey

Miezi sita ya vita nchini Ukraine haya ni baadhi ya yaliyofanywa na WFP

Hii leo imetimia miezi sita rasmi tangu kuanza kwa vita baina ya Ukraine na Urusi baada ya Urusi kuivamilia Ukraine vita ambayo si tu imeleta madhara na maafa kwa Ukraine bali dunia kwa ujumla ikiwemo kupandisha bei za mafuta na chakula. Katika siku hiii tuangalia machache yaliyofanywa na moja tu la mashirika mengi ya Umoja wa Mataifa lile la Mpango wa Chakula duniani WFP katika kuwasaidia wananchi wa Ukraine.

Sauti
3'5"
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres akiwa katika meli ya majaribio kupitia bahari ya Marmara nchini Uturuki ili kumtazama Kamanda Jasiri.
UN Photo/Mark Garten

Kama ilivyo kwa Nafaka, Mbolea pia inahitajika katika soko la dunia: Guterres

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres hii leo nchini Uturuki ametembelea na kukagua shughuli zinazoendelea za ukaguzi wa meli kutoka Ukraine zenye shehena ya nafaka zinazoenda kuuzwa katika soko la kimataifa na kupongeza muungano wa wakaguzi hao kutoka Ukraine , Urusi, Uturuki na Umoja wa Mataifa kwa kazi nzuri wanayofanya ambayo itasaidia dunia kuondokana na upungufu wa chakula uliosababisha bei kupanda na kuathiri zaidi nchi zinazoendelea zenye rasilimali chache kuweza kukidhi mahitaji ya wananchi wake. 

Katibu Mkuu Antonio Guterres akipanda meli ya Kubrosliy huko Odesa, Ukraine.
UN Photo/Mark Garten

Kila meli inayoondoka Odesa imebeba matumaini- Guterres

Leo hii Odesa ni zaidi ya bandari ya kusafirisha, shehena, amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres hii leo alipotembelea bandari hiyo iliyoko Ukraine, kujionea upakiaji wa shehena za nafaka na chakula kufuatia makubaliano ya kusafirisha nafaka kupitia Bahari Nyeusi, makubaliano yaliyowezesha kuanza kusafirishwa kwa bidhaa hizo kwenda soko la dunia licha ya uvamizi unaoendelea wa Urusi nchini Ukraine. 

Mwelekeo wa shehena za vyakula kutoka Ukraine.
UN News

Hatimaye meli yenye shehena ya ngano yaondoka Ukraine kuelekea Pembe ya Afrika

Meli ya kwanza ya Ukraine yenye na unga wa ngano wa Ukraine utakaosambazwa na shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani, WFP kwenye operesheni zake za kibinadamu imeondoka bandari ya Yuzhny nchini Ukraine hii leo,  hatua ambayo imetajwa kuwa ya muhimu zaidi na inayohitajika ya kuondoa nafaka kwenye taifa hilo lenye mzozo kuelekea nchi zinazokumbwa na janga la uhaba wa chakula duniani.