Meli iliyobeba msaada wa chakula kwa ajili ya wananchi wa Ethiopia yatia nanga Djibout
Hatimaye meli iliyokodiwa na Umoja wa Mataifa iliyokuwa imepakia tani 23,000 za ngano kutoka Ukraine inayopeleka kwa mamilioni ya watu wenye uhitaji wa chakula nchini Ethiopia ilitia nanga katika nchi jirani ya Djibouti.