Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mashariki ya Kati

Mahakama ya Kimataifa ya Haki ikisikiliza kessi ya Afrika Kusini dhidi ya Israel mjini The Hague. (Maktaba)
ICJ-CIJ/ Frank van Beek

ICJ yaitaka Israeli iepushe mauaji ya kimbari Gaza

Mahakama ya Kimataifa ya Haki, ICJ hii leo imeamua kuwa Israel lazima ichukue hatua zote za kuzuia vitendo vya mauaji ya kimbari katika mashambulizi yake dhidi ya wapalestina huko, Gaza, uamuzi unaofuatia shauri lililowasilishwa na Afrika Kusini la kutaka Mahakama hiyo ya Umoja wa Mataifa ichukue hatua za awali kwa mujibu wa Mkataba wa kimataifa wa kuepusha mauaji ya kimbari wa mwaka 1948. 

Sauti
2'13"
Mashambulizi ya anga yaharibu majengo katika Ukanda wa Gaza. (Maktaba)
© UNRWA/Ashraf Amra

Raia 25,000 wamepoteza maisha katika vita Gaza na mahitaji ya kibinadamu yanazidi kuongezeka: UN

Mashambulizi makubwa ya mabomu yanayofanywa na Israel Gaza yameendelea tena leo sanjari na maroketi yanayovurumushwa na makundi yenye silaha ya Kipalestina kuelekea Israel, wakati wahudumu wa kibinadamu wa Umoja wa Mataifa wakiripoti kuuawa kwa watu zaidi ya 25,000 Gaza tangu kuanza kwa machafuko hayo mapya Oktoba 7 mwaka jana na mahitaji ya kibinadamu yakiongezeka kila uchao.

Sauti
2'22"
Msichana mdogo amelazwa katika hospitali ya Al-Quds huko Gaza.
© UNICEF/Eyad El Baba

Hali ya Gaza ni zahma juu ya zahma: Mashirika ya UN

Mashirika ya kibinadamu ya Umoja wa Mataifa leo yameeielezea hali inayoendelea Gaza siku 105 baada ya kuzuka vita mpya baina ya wapiganaji wa Hamas na vikosi vya Israel, kuwa ni zahma juu ya zahma. Watu zaidi ya milioni 1.7 wametawanywa huku hofu ya milipuko ya magonjwa, janga la njaa na vifo zaidi likitawala.

Sauti
2'
Malori yaliyosheheni msaada wa kibinadamu yakijiandaa kuingia Gaza kupitia kivuko cha Rafah
© UNICEF/Eyad El Baba

Mashirika ya UN yaomba kufunguliwe njia nyingine ya kufikisha misaada Gaza

Zikiwa ni zaidi ya siku 100 tangu kuibuka upya kwa mzozo huko Mashariki ya Kati, mashirika ya Umoja wa Mataifa hii leo yametoa taarifa inayoelezea kuongezeka kwa hatari ya baa la njaa na milipuko ya magonjwa ya kuambukiza huku yakisisitiza muarobaini pekee kwa sasa ni kuruhusu njia mpya za kuingiza misaada ya kwenda kutatua changamoto zinazowakabili wananchi walioko Gaza. 

Sauti
3'34"
Watu waliojeruhiwa wakisubiri kutibiwa katika hospitali ya Al Shifa mjini Gaza. (Maktaba)
© WHO

Mzozo Gaza: Hospitali zazidi kuzidiwa uwezo, wagonjwa sakafuni

Ikiwa leo ni siku ya 93 tangu mapigano yaanze huko Ukanda wa Gaza kati ya jeshi la Israel na wanamgambo wa kipalestina waliojihami, likiwemo kundi la Hamas, mashirika ya Umoja wa Mataifa ya usaidizi wa kiutu yanazungumzia uwepo wa idadi kubwa ya vifo miongoni mwa wanawake na watoto huku yakisihi timu za madaktari ziruhusiwe kuingia eneo la Gaza ili ziendelee na jukumu la kuokoa maisha. 

Sauti
2'16"
Wanawake huko Gaza wakisafirisha vifurushi vya chakula vinavyosambazwa na WFP. (Maktaba)
© WFP/Ali Jadallah

OHCHR yataka uchunguzi Gaza kufuatia madai ya ukatili wa kingono wakati wa shambulio la Hamas

Kamishina Mkuu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa Volker Türk leo amelaani vikali ukiukaji mkubwa wa haki wa kingono dhidi ya Waisraeli unaodaiwa kutekelezwa na wanamgambo wa Hamas wakati wa mashambulizi yao ya kigaidi kusini mwa Israel tarehe 7 Oktoba, huku wahudumu wa kibinadamu huko Gaza wakionya kuhusu hali mbaya ya raia, kutokana na kunaendelea kwa mashambulizi ya mabomu na watu kutawanywa eneo la Kusini.

Sauti
1'53"