Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Burundi

Watoto wakimbizi wa ndani huko Ituri nchini DRC.
UN/Eskinder Debebe

Mauaji na utekaji nyara wa watoto kwenye maeneo ya vita vilishamiri mwaka 2021- Ripoti

Mwaka wa 2021  umeshuhudia mchanganyiko wa mwendelezo hatari wa mizozo, mapinduzi ya kijeshi sambamba na mizozo mipya na ile iliyodumu muda mrefu na ukiukwaji mkubwa wa sheria za kimataifa, vyote ambavyo kwa pamoja vimekuwa na madhara makubwa kwa watoto duniani kote, amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres kupitia ripoti yake ya mwaka kuhusu Watoto kwenye mizozo ya kivta, ripoti ambayo imechapishwa hii leo.

Familia kutoka Eritrea ikiwa kwenye kituo cha muda Romani wakisubiriwa kuhamishwa hadi Netherlands.
© UNHCR/Stefan Lorint

Idadi ya wasaka hifadhi nchi ya tatu kuongezeka 2023

Zaidi ya wakimbizi milioni 2 mwaka ujao WA 2023 watahitaji kuhamishiwa nchi ya tatu ikiwa ni ongezeko kwa asilimia 36 ikilinganishwa na mahitaji ya mwaka huu ambayo ni wakimbizi milioni 1.5 pekee, limesema shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR kupitia tathmini ya makadirio ya kuhamia nchi ya tatu kwa mwaka 2022.

Vital Bambanze (kulia) mwakilishi wa jamii ya watwa nchini Burundi akiwa kwenye majadiliano na washiriki wengine wakati wa mkutano wa 21 wa jukwaa la Kudumu la Umoja wa Mataifa la watu wa asili, UNPFII mwezi Aprili 2022 jijini New York, Marekani.
UN/ Flora Nducha

Nuru Burundi kwa haki za jamii ya Watwa

Mkutano wa 21 wa Jukwaa la Kudumu la Umoja wa Mataifa la watu wa asili, UNPFFII likiwa limeingia siku ya tatu kwenye makao makuu ya Umoja huo jijini New York, Marekani, washiriki kutoka Burundi wameieleza Idhaa ya Kiswahili ya  Umoja wa Mataifa juu ya hatua zinazoendelea kuchukuliwa ili kuhakikisha haki za binadamu za jamii ya asili aina ya watwa zinazingatiwa.