Wachuuza nyanya na mboga mboga ili kujinasua kutoka lindi la umaskini
Umoja wa Mataifa na wadau wake unachagiza maendeleo ili kubadili maisha ya wakazi wa dunia hii ikiwemo kutokomeza umaskini. Na ndio maana chombo hicho kilipitisha malengo ya maendeleo endelevu,. SDGs ambapo lengo namba moja ni la kutokomeza umaskin ifikapo mwaka 2030. Ni kwa kuzingatia hilo wanawake wa wilaya ya Lwengo, Kusini mwa Uganda nao wameamua kujifunga kibwebwe kuweza kutokomeza umaskini. Wameanzisha soko lao ambalo linauza bidhaa mbalimbali za matunda kama vile nyanya , na mboga za majani. Siraj Kalyango alivinjari eneo hilo na kukuandalia makala ifuatayo.