Kituo cha amani DR Congo chakabili habari potofu na za uongo
Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, kituo kilichojengwa na ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa
Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, kituo kilichojengwa na ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa
Mwanamuziki Innocent Balume, al maaruf Innoss’B ametangazwa kuwa muungaji mkono wa ngazi ya juu wa shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula duniani, WFP katika kusongesha milo yenye afya na lishe bora nchini mwake Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC.
Juhudi na ushirikiano wa pamoja wa wahudumu wa afya, vituo na Jamii, vimefanikisha kukomesha mlipuko wa kipindupindu uliozuka nchini Zambia kwa mujibu wa Shirika Umoja wa Mataifa la Afya Duniani WHO nchini Zambia, ambalo limeeleza kwamba ugunduzi wa mapema na matibabu husaidia kukabiliana na ugonjwa huo na kupunguza idadi ya vifo.
Jioni moja Philta Samazimva alilalamika ghafla tumbo kuuma, baada ya kuharisha sana, mama yake mzazi Hildar Samazimba alimpeleka kliniki.
Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini UNMISS kwakushirikiana na wadau wake wamefun
Ikiwa leo ni Siku ya Kimataifa ya Mshikamano na Wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa Walio vizuizini na wasiofahamika waliko, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametoa wito kwa ulimwengu kuenzi ujasiri na kujitolea kwa wafanyakazi wanaotoa huduma za kibinadamu kila mahali kokote waliko kwa kuahidi kuwalinda na kuwaunga mkono wanaposaidia kujenga dunia yenye amani zaidi na ya utu kwa ajili ya watu wote. Assumpta Massoi na maelezo zaidi.
Leo ni siku ya maji duniani chini ya kauli mbiu Maji kwa amani ambapo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres katika ujumbe wake kwa siku hii amehimiza nchi kuhakikisha zinashirikiana na kuwa na makubaliano ya kutumia vyanzo vya maji.
Katika ujumbe wake huo Guterres ameeleza kuwa mpaka sasa ulimwenguni “Nchi 153 zinashirikiana vyanzo vya maji lakini ni nchi 24 pekee zenye makubaliano kwa vyanzo vyao vyote vya maji wanavyoshirikiana.”
Wahudumu wa afya Gaza wanafanya kazi mchana kutwa na usiku kucha wakihaha kuokoa Maisha ya wagonjwa na majeruhi katika hospitali chache zilizosalia zikifanyakazi bila kutia chochote tumboni kwa mujibu wa shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO.
WHO inasema wafanyakazi hao wanaolazimika kufanyakazi saa 24 kuokoa maisha ya watu kama ambavyo wanakosa vifaa muhimu na vitendeakazi vingine vivyo hivyo wanakosa chakula cha kutosha kama ilivyo kwa maelfu mengine ya raia wa Gaza.
Katika kuhakikisha watoto wanapata chanjo zote zinazohitajika, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF nchini Yemen limekuja na mbinu ya kutumia watoto kuhamasisha jamii kupeleka watoto kupata chanjo.
Mtoto Leen mwenye umri wa miaka 10 kutoka nchini Yemen, anasema kupitia mpango wa ufadhili wa mtoto, programu inayotumia watoto kwenda kuhamasisha jamii kupata chanjo ili wawe na afya bora amefanikisha watoto 150 kupata chanjo katika jamii yake.
Hali ya uhakika wa kupata chakula huko Gaza, ni tete na baa la njaa linanyemelea kwenye majimbo ya kaskazini mwa eneo hilo imesema ripoti mpya ya hali ya chakula Gaza iliyotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo, FAO, likisema jawabu la kuondokana na hali hiyo ni amani.
Timu kutoka Kurugenzi ya Haki Sheria ya Jeshi la Ulinzi wa Wananchi wa Sudan Kusini (SSPDF) mwishoni mwa wiki kwa usaidizi wa Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini (UNMISS), imehitimisha tathmini yake katika Kaunti ya Maridi jimboni Equatorial Magharibi kutathmini kesi zinazohusisha wanajeshi wa nchi hiyo.
Tathimini itawezesha kufunguliwa mashtaka kwa askari wa jeshi ambao wanashukiwa kufanya uhalifu mkubwa, ikiwa ni pamoja na unyanyasaji wa kingono na aina nyingine za unyanyasaji wa kijinsia.