Kila mmoja anajukumu la kumlinda mwenzie na ukimwi
Katika siku ya ukimwi duniani wito umetolewa kwa kila mtu kubeba jukumu la kujilinda na kuwalinda wengine na maambukizi mapya ya ukimwi.
Katika siku ya ukimwi duniani wito umetolewa kwa kila mtu kubeba jukumu la kujilinda na kuwalinda wengine na maambukizi mapya ya ukimwi.
Wananchi milioni 32 wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo wameshiriki hii leo katika uchaguzi mkuu ulioshuhudia wagombea 11 wakiwania wadhifa wa urais akiwemo rais anayeondoka madarakani Joseph Kabila na mpinzani wake mkuu Etienne Tchisekedi.
Wakati ripoti ya shirikika la Umoja wa Mataifa la kupambana na HIV na ukimwi UNAIDS iliyotolewa leo imesema ingawa maambukizi mapya yamepungua na vifo vitokanavyo na ukimwi vimepungua lakini matunzo kwa waathirika la lishe ni muhimu sana katika kuokoa maisha ya wagonjwa.
Mamia ya wakimbizi ambao walihama makwao kutokana na mzozo wa uchaguzi ulioikumba Ivory Coast wameanza kurejea nyumbani kwa usaidizi wa shirika la kimataifa la uhamiaji IOM.
Shirikisho la kimataifa la maradhi ya Kisukari IDF na shirika la afya duniani WHO wanasema maradhi ya kisukari yanaweza kuzuuilika kwa watu kuzingatia masharti ikiwemo kula vyakula vinavyofaa, kufanya mazoezi, kupungza unene na kuepuka matumizi ya tmbaku.
Shirika la maendeleo la Umoja wa Mataifa UNDP limezindua ripoti ya maendeleo ya binadamu mwaka 2011 nchini Tanzania. Washirika mbali mbali walihudhuria mkutano huo wakiwemo Dr Paniel Lyimo, katibu mkuu wa kudumu kwenye ofisi ya waziri mkuu wa Tanzania ambaye alikuwa mgeni rasmi, Dr.
Mwakilishi maalmu wa Umoja wa Mataifa nchini Somalia balozi Augustine Mahiga amesema ana matumaini operesheni za pamoja za kijeshi za serikali ya mpito na Kenya dhidi ya wanamgambo wa Al-Shabaab zikikamilika hali ya amani itakuwa shwari Somalia.
Huko Burundi, Jeshi la nchi hiyo limesema kwamba halitavunjika moyo licha ya tukio la hivi karibuni nchini Somalia ambako walinda amani wake katika kikosi cha Amisom waliuwawa wiki iliopita. Hata hivo giza linaendelea kutanda kuhusu idadi ya wanajeshi waliouwawa.
Mwakilishi maalumu wa Umoja wa Mataifa nchini Somalia Balozi Augstine Mahiga leo amethibitisha kwamba vikosi vya jeshi la Kenya vimeingia Somalia.
Serikali ya Tanzania imeitaka jumuiya ya kimataifa kuongeza juhudi na kunyoosha mkono zaidi kusaidia kunusuru maisha ya mamilioni ya watu nchini Somalia.