Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Tanzania yaitaka jumuiya ya kimataifa kuongeza msaada Somalia

Tanzania yaitaka jumuiya ya kimataifa kuongeza msaada Somalia

Pakua

Serikali ya Tanzania imeitaka jumuiya ya kimataifa kuongeza juhudi na kunyoosha mkono zaidi kusaidia kunusuru maisha ya mamilioni ya watu nchini Somalia.

Somalia ambayo imekuwa katika vita vya wenyewe kwa wenyewe kwa zaidi ya miongo miwili sasa inakabiliwa pia na tatizo kubwa la njaa, utapia mlo kwa watoto na kame.

Waziri wa mambo ya nje wa Tanzania ameyasema hayo kwenye mdahalo uliofanyika leo nchini Tanzania na kujumuisha wadau mbalimbali yakiwemo mashirika ya Umoja wa mataifa. Mwandishi wa Idhaa hii George Njogopa alikwepo na kuandaa taarifa hii.

(RIPOTI YA GEORGE NJOGOPA)