Bahari – mdau wetu mkubwa dhidi ya mabadiliko ya tabianchi – inakabiliwa na tatizo kubwa. Kusongesha kwa kasi majawabu ya kulinda sayari yetu na kufungua sura mpya ya hatua kwa ajili ya bahari, viongozi wa dunia na wachechemuzi wa bahari wanakutana Lisbon, Ureno kuanzia 27 Juni hadi 1 Julai, kwenye mkutano wa pili wa UN kuhusu Bahari.
Hapa, Habari za UN inajikita katika hatua zote; tutakupatia kile kinachojiri kila siku kwenye Mkutano huo; mahojiano, podikasti, makala vikimulika simulizi za kibinadamu kwenye harakati za kimataifa ili #kulindabahari

Hamasika

Makala

Photo of two boats

Mambo 5 ya mkutano wa UN kuhusu Bahari

Bahari ni mfumo ikolojia mkubwa zaidi unaodhibiti tabianchi, na kuwa chanzo cha kipato kwa mabilioni ya watu. Lakini afya yake iko hatarini. Si kila siku itatupatia fursa ya kuilinda, lakini kila siku itatupatia fursa ya kulinda.
Photo of a dog with a dog treat

Kutotupa taka: Mabaki ya samaki yageuzwa chakula cha mbwa

Hakuna shaka kuwa upotevu na utupaji wa chakula, vimekuwa vikikwamisha uendelevu wa mifumo yetu ya chakula. Katika kukabili hilo, sekta ndogo za biashara duniani kote zimejikita kusaka mbinu endelevu za kusimamia taka.
Photo of the co-hosts of the Ocean Conference

"Kwa pamoja tukidhi mahitaji ya kutunza bahari yetu", Wasihi wenyeji wenza

Ana Paula Zacarias na Martin Kiman wanaelezea vile wapendavyo bahari na harakati zao za kuhakikisha  uhifadhi na matumizi endelevu ya bahari na rasilimali za bahari kwa ajili ya maendeleo endelevu kwa wote.

Habari mpya

Pata Habari za Mkutano kuhusu Bahari

Fahamu zaidi kuhusu habari zetu kila siku kutoka kwenye Mkutano ikiwemo mahojiano, podikasti, makala vyote vikimulika simulizi za kibinadamu kwenye harakati za kimataifa ili #kulindabahari

 

Je wajua

Ukubwa wa bahari ni asilimia 70 ya eneo lote la uso wa dunia, na ni makazi ya takribani asilimia 80 ya viumbe vya dunia? Ni eneo kubwa zaidi la eneo chini ya anga.

Kijarida

Kuhusu Mkutano

photo of fishermen with a mesh net use tapping techniques to move schools of fish

Mkutano wa UN kuhusu Bahari

Mkutano kuhusu Bahari unaoandaliwa kwa pamoja na serikali za Kenya na Ureno, unafanyika wakati muhimu kwa kuwa dunia inasaka majawabu ya kutatua matatizo yaliyoota mizizi na ambayo yameibuliwa na janga la COVID-19, majawabu ambayo yatahitaji marekebisho makubwa ya kimuundo na suluhu za pamoja zinazozingatia SDGs. Kuchagiza hatua hizo, Mkutano wa Bahari unasaka kuchagiza kasi ya suluhu bunifu za kisayansi zinazohitajika kwa lengo la kufungua ukurasa mpya wa hatua za kimataifa kwa ajili ya bahari.

Learn more about the Ocean Conference

Plastic pollution in the world's oceans is threatening marine life

Maisha chini ya maji

Bahari ni kitu maarufu kwenye sayari, ikifunika tarkibani theluthi 3 ya Dunia na ni muhimu kwa uhai wa sahari hii. Kama ambavyo mtu hawezi kuishi bila kuwa na mapafu yenye afya, vivyo hivyo Dunia haiwezi kuwa hai bila bahari yenye afya. Bahari ni mapafu ya dunia, ikizalisha hewa ya oksijeni kwa ajili ya uhai na kufyonza hewa ya ukaa na taka. Bahari inahifadhi na kufyonza hewa ya ukaa kutoka duniani, ilhali mimea ya baharini inazalisha oksijeni inayohitajika kwa ajili ya uhai.

Loading...