UDADAVUZI: Je, UN inaunga mkono vipi harakati za Haiti kukabiliana na ghasia na ukosefu wa utulivu?
Haiti inakabiliwa na ghasia zilizoenea za magenge ya uhalifu, taasisi za nchi hiyo ziko kwenye hatihati ya kuporomoka na raia wake wanakabiliwa na changamoto za kila siku za kuweza kuishi. Hata hivyo, katikati ya janga hili la usalama na kibinadamu, Umoja wa Mataifa unaendelea kutoa msaada muhimu kwa watu walioathirika.