Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Makala Maalum

Lori likiwa limejaa chupa za maji ya kunywa  likielekea Al Arish mji ulio kilometa 32 kusini mwa mpaka wa Gaza
© UNICEF/Mohamed Ragaa

Udadavuzi: Kuna nini ndani ya msafara wa misaada kwenye kivuko cha Gaza

Chini ya kilomita moja kutoka Gaza, vibao vya kuengeshean chakula, mafuta, maji, na dawa ni miongoni mwa mamia ya tani za misaada ya kuokoa maisha iliyopakiwa kwenye msafara mrefu wa malori yakiwa yamesimama kwenye upande wa Misri wa kivuko cha mpakani ch a Rafah, huku madereva wakisubiri ruksa ya Israel ili waweze kufikia Wapalestina milioni 2.3 waliozingirwa na walionaswa katika mzozo wa vita vinavyoendelea.

Jengo liliporomoka huko Gaza.
© UNRWA/Mohammed Hinnawi

Mgogoro Mashariki ya Kati: Umoja wa Mataifa unasaidia vipi?

Umoja wa Mataifa umekuwa ukifanya kazi katika eneo la Mashariki ya Kati muda wote ili kupunguza mzozo wa Israel na Palestina kwa kuwashirikisha wahusika wakuu na kutoa msaada wa dharura kwa raia walioko mashinani. 

Wakati mzozo huo ukiongezeka huku kukiwa na ongezeko la ghasia, kizuizi kamili cha chakula, maji, na huduma muhimu kiliwekwa na Israel huku ripoti zikiibuka kuhusu operesheni za ardhini za Israel huko Gaza, ambako kuna wakazi zaidi ya milioni mbili.

Mradi wa FAO nchini Thailand wa kupunguza upotevu wa chakula na taka kuna jukumu muhimu katika kubadilisha mifumo ya kilimo na chakula.
© FAO/Alisa Suwanrumpha

Mradi wa FAO wa kupunguza upotevu na utupaji wa chakula nchini Thailand wainua kipato cha wafanyabiashara

Kupunguza upotevu na utupaji wa chakula kuna jukumu muhimu katika kubadilisha mifumo ya kilimo na chakula. Kati ya malengo 17 ya Maendeleo endelevu ya Umoja wa Mataifa ambayo yanafikia kilele mwaka 2030 lengo namba 2 linahimiza kutokomeza njaa, lengo namba 8 linahimiza kazi nzuri na ukuaji wa kiuchumi na lengo namba 12 lina himiza utumiaji na uzalishaji wenye kuwajibika lengo likiwa kuwa na mifumo endelevu ya utumiaji wa rasilimali. Malengo yote haya yanaenda sambamba na harakati za kupunguza upotevu na utupaji wa chakula.

Amadou Jobe, mhamiaji ambaye alirejea Gambia kutoka Ulaya, akiangalia bahari ya Pasifiki kutoka pwani ya Gambia.
UN News/ Hisae Kawamori

Sitamani tena kuzamia kwenda Ulaya: Manusura kutoka Gambia

Kila mwaka maelfu ya wahamiaji kutoka maeneo mbalimbali ikiwemo Afrika hujaribu kufika Ulaya wakivuka bahari ya Mediterania kwa lengo la kwenda kusaka maisha bora lakini safari hiyo inaelezwa kuwa ni hatari sana kwani maelfu ya watu hufa maji au kutoweka. Evariste Mapesa anatupeleka nchini Gambia kusikia simulizi ya kijana ambaye chupuchupu apoteze maisha. 

 

Sauti
3'19"
Kina mama kutoka Kenya ambao wananyonyesha watoto wao, wakiwatumbuiza wageni kwenye uzinduzi wa wiki ya kuelimisha umma kuhusu umuhimu wa kunyonyesha.
UN News/Thelmaa Mwadzaya

Unyonyeshaji wa watoto maziwa ya mama huimarisha afya yao na ya mama - Wanaharakati Kenya

Kulingana na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF, watoto wanaonyonya maziwa ya mama pekee katika miezi sita ya mwanzo ya uhai wanapiga hatua nzuri za kiafya kama anavyoelezea Kasha Mutenyo kwamba, "umuhimu wa kwanza wa kunyonyesha ni kwamba afya ya mtoto inaimarika na haugui kila wakati. Sio ghali, ni salama na hauhitaji vifaa vyovyote kumnyonyesha mtoto. Pia inamsaidia mama kupanga uzazi.”

Sauti
6'58"