Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Neno La Wiki

UN

JIFUNZE KISWAHILI : Mzishi

Leo Onni Sigalla, Mhariri Mwandamizi wa Baraza la Kiswahili Taifa Tanzania, BAKITA, anafafanua maana ya neno Mzishi, akisema katika hali ya msiba ndio kuna mzishi. Huyu ni ndugu au jamaa anayeshughulikia mazishi ya mtu. Mzishi anashughulikia mazishi ya mtu na ni mtu ambaye anaweza kuwa karibu na mtu wakati wa shida na raha.

Sauti
52"
UN

Neno la Wiki - Msagaliwa

Hii leo katika kujifunza lugha ya Kiswahili tunakwenda nchini Tanzania katika Baraza la Kiswahili la Taifa, BAKITA ambako Mhariri Mwandamizi Onni Sigalla anafafanua maana ya neno Msagaliwa.

Anasema huyu ni mwanaume au mvulana ambaye anapenda zaidi kuwa na wanawake muda mwingi au muda wowote. Anasema si ugonjwa bali inatokana na malezi au tatizo la kisaikolojia anapenda kuzungumza na watu wa jinsia nyingine. Wingi wake ni wasagaliwa. Msikilize kwa kina zaidi.

Sauti
59"