Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Makala

UNODC/Ioulia Kondratovitch

Vituo vya kusaidia waathirika wa madawa ya kulevya ni msaada mkubwa

Hii leo ikiwa ni siku ya kupiga vita matumizi ya madawa ya kulevya duniani, vituo vya kusaidia waathirika wa madawa hayo vimekuwa msaada mkubwa wakati huu ambapo Umoja wa Mataifa unasema ya kwamba watu milioni 35 ulimwenguni kote wana matatizo yatokanayo na matumizi ya madawa hayo ilhali ni mtu 1 tu kati ya 7 ndiye anayepata matibabu. Assumpta Massoi na ripoti kamili.

Sauti
6'5"
FAO

Mabadiliko ya tabianchi ni janga kwa wafugaji Uganda

Mabadiliko ya tabianchi ni janga ambalo linaikabili dunia hii leo ambapo Umoja wa Mataifa na washirika wake kupitia lengo nambari 13 la ajenda ya mwaka 2030 ya maendeleo endeleve au SDGs, wamekuwa msatari wa mbele kubonga bongo ili  kutafuta suluhisho ikiwa ni pamoja na  kuhamisha serikali na asasi mbalimbali kuweza kutafuta njia mbadala ya kupambana na janga hili.

Sauti
3'48"
UN News/Patrick Newman

Nilipitia changamoto za wanaume lakini nikawashawishi na kushinda-Mboni Mhita.

Kwa muda mrefu jamii mbalimbali zimeendelea kukumbatia mfumo dume ambapo wanawake wamekuwa wakipewa nafasi ya nyuma baada ya wanaume, iwe katika elimu, maamuzi katika jamii na hata katika nafasi za uongozi. Ndiyo maana lengo namba 5 la maendeleo endelevu linasisitiza kuhusu usawa wa kijinsia ambapo kila mtu anatakiwa kuwa na haki ya kushiriki katika masuala mbalimbalimbali ya jamii yake bila kujali jinsia yake.

Sauti
4'13"
UNICEF/Mulugeta Ayene

 IFAD yawajenga mnepo wakulima nchini Ethiopia.

Zaidi ya watu bilioni moja kote duniani wanaishi katika maeneo ambayo yana uhaba mkubwa wa maji, na watu wengine wapatao bilioni 3.5 watakabiliwa na changamoto kubwa ya uhaba wa maji ifikapo mwaka 2025 kwa mujibu wa takwimu za shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo FAO na shirika la maendeleo ya kilimo IFAD.

Sauti
3'6"
© UNHCR/Jordi Matas

Mwanafunzi mkimbizi wa DRC atunukiwa tuzo Uganda

Mamilioni ya watu wameendelea kufungasha virago kila uchao kwenda kusaka usalama wakikimbia vita, mateso, mauaji, njaa na sambabu zingine mbalimbali. Japo wakimbizi hawa wanaonekana mzingo machoni mwa wengi Umoja wa Mataifa unasema dunia ikiwakumbatia itaoona mchango wao na faida yao.

Sauti
4'7"
Isaya Yunge

Vijana changamoto zisiwakatishe tamaa bali ziwape chachu ya kusonga mbele- Isaya

Umoja wa Mataifa hivi sasa unataka vijana ndio wawe mstari wa mbele katika kufanikisha malengo ya maendeleo endelevu, SDGs. Ndio maana kila uchao kupitia mashirika yake mbalimbali chombo hicho chenye wanachama 193 kinapaza sauti kwa vijana kushiriki na kushirikishwa katika kila utekelezaji wa malengo hayo kuanzia kutokomeza umaskini, kusongesha amani, afya na hata  ubia wa  maendeleo.

Sauti
4'38"
Arne Hoel/World Bank

Benki ya Dunia na Uganda zashirikiana kuokoa eneo oevu la Mabamba

Maeneo oevu ni maeneo yenye bayonuai ya kipekee ya maji, mimea na viumbe na ambapo zaidi ya uzuri wake, yana manufaa ya kiuchumi na kijamii.

Hata hivyo Benki ya Dunia inasema kuwa maeneo haya yanazidi kukumbwa na zahma kutokana na matumizi yake ya asili kupokwa na shughuli za binadamu kama vile kilimo na uvuvi usio endelevu. Mathalani nchini Uganda, eneo oevu la Mabamba nalo liko hatarini na sasa hatua zinachukuliwa kulihifadhi.

Je ni zipi hizo, Assumpta Massoi anasimulia kwenye makala hii.

 

 

Sauti
4'7"
UN /Marie Frechon

Ingawa kuna changamoto angalau Kenya imechukua hatua kutulinda watu wenye ulemavu wa ngozi- Mbunge Mwaura

Tarehe 13 mwezi Juni ya kila mwaka ni siku ya kimataifa ya kuhamasisha jamii kuhusu haki za watu wenye ulemavu wa ngozi. Siku hii inaadhimishwa kwa kuzingatia changamoto wanazokabiliana nazo kundi hilo ikiwemo kutengwa, kunyanyapaliwa na pia hata kuuawa kwa fikra potofu ya kwamba viungo vyao vinaweza kutumika kwa ajili ya utajiri.

Nchini Kenya, moja ya mataifa ambayo kundi hilo limekumbwa na changamoto, tayari kuna watetezi ndani ya kundi hilo na miongoni mwao ni Isaac Mwaura, mlemavu wa ngozi ambaye ni wa kwanza kuchaguliwa kuwa mbunge kwenye bunge la Kenya.

Sauti
3'31"