WFP: kuna uhaba wa chakula mashariki mwa DRC
Umoja wa Mataifa unasema wananchi milioni 23.4 sawa na robo ya wananchi wote takriban milioni 96 wa Jamhuri ya Kidemokrasia Kongo DRC, wanakabiliwa na njaa. Wengi wa wananchi hao wanaishi katika hali duni na yenye msongamano wa watu wasio na uwezo wa kupata chakula, huduma za afya na elimu.