Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Ugawaji wa dharura wa chakula unaendelea Mashariki mwa DRC. (Maktaba)
© WFP/Michael Castofas

WFP: kuna uhaba wa chakula mashariki mwa DRC

Umoja wa Mataifa unasema wananchi milioni 23.4 sawa na robo ya wananchi wote takriban milioni 96 wa Jamhuri ya Kidemokrasia Kongo DRC, wanakabiliwa na njaa. Wengi wa wananchi hao wanaishi katika hali duni na yenye msongamano wa watu wasio na uwezo wa kupata chakula, huduma za afya na elimu.

Janga la usalama la hivi majuzi nchini Haiti limefanya iwe vigumu kwa PAHO kusaidia mamlaka za afya kusaidia watu waliokimbia makazi yao katika eneo la mji mkuu wa Port-au-Prince.
© PAHO/David Lorens Mentor

Haiti: Kuongezeka kwa ghasia na misukosuko ya kiuchumi inazidisha janga la njaa – FAO

Haiti iko katika hali mbaya ya mgogoro wa kibinadamu, na karibu nusu ya idadi ya watu wana uwezekano wa kukabiliwa na uhaba mkubwa wa chakula, kulingana na uchambuzi wa hivi karibuni wa Uainishaji wa Uhakika wa Chakula (IPC). Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo (FAO) linatahadharisha kuhusu athari mbaya ikiwa hatua za haraka hazitachukuliwa kushughulikia sababu kuu za mgogoro huu.

Wanawake nchini Tanzania wakivuna seaweed kama sehemu ya mradi wa kilimo bora cha hali ya hewa.
UN Women/Phil Kabuje

Mwani una nafasi kubwa katika kufanikisha SDGs- Ripoti ya UNCTAD

Utafiti mpya uliotolewa na Kamati ya Umoja wa Mataifa ya Maendeleo ya Biashara, UNCTAD inaonesha Tanzania kuwa inaongoza barani Afrika kwa kilimo na uuzaji nje ya nchi wa zao la mwani, huku wanawake wakulima wa zao hilo nchini Kenya wakiwa mstari wa mbele kuondokana na matumizi ya Kamba za plastiki katika kilimo cha zao hilo linalozidi kupata umaarufu duniani kila uchao kutokana na faida zake za kiafya.

Alec Collett,alikuwa mtumishi wa UN alikamatwa na kuuawa akiwa katika kazi za UN
Picha ya UN /Milton Grant

Tekelezeni kikamilifu mkataba wa mwaka 1994 wa kuwalinda wafanyakazi wa UN - Guterres

Ikiwa leo ni Siku ya Kimataifa ya Mshikamano na Wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa Walio vizuizini na wasiofahamika waliko, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametoa wito kwa ulimwengu kuenzi ujasiri na kujitolea kwa wafanyakazi wanaotoa huduma za kibinadamu kila mahali kokote waliko kwa kuahidi kuwalinda na kuwaunga mkono wanaposaidia kujenga dunia yenye amani zaidi na ya utu kwa ajili ya watu wote. 

Sauti
1'45"